Monday 8 September 2014

WATAWA WATATU WAUAWA BURUNDI


Undated handout picture of Olga Raschietti
Olga Raschietti amekaa miaka mingi Afrika ya Kati

Polisi nchini Burundi imesema watawa watatu, watu wazima wamebakwa na kuuawa kwenye makazi yao nje ya mji mkuu Bujumbura.

Watawa wawili waliuawa siku ya Jumapili huku mtawa wa tatu ambaye mwili wake uligundulika mapema siku ya Jumatatu ulikutwa kichwa chake kikiwa kimekatwa.

Watawa hao wametajwa kuwa Lucia Pulici, mwenye umri wa miaka 75, Olga Raschietti, miaka 82, na Bernadetta Boggian, mwenye miaka 79.

Serikali imesema anayeshukiwa kufanya mauaji hayo katika shambulio la kwanza alionekana akikikmbia makazi ya watawa hao huku akiwa na kisu mkononi.

Dayosisi ya Italia huko Parma imesema watawa hao wameuawa kukiwa na jaribio la ujambazi.

Hatahivyo, polisi wa Burundi, wamesema nia yao haijulikani ni nini, kwani hakuna pesa zozote zilizoibiwa.

Mwaka 2011, mtawa kutoka Croatia na mfanyakazi wa kutoa misaada wa Italia waliuawa katika jaribio la wizi kaskazini mwa Burundi.

Chanzo: BBC 
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment