Tuesday 9 September 2014

APPLE YAZINDUA iPHONE YENYE UKUBWA ZAIDI



Apple iPhones

Kampuni ya Apple imetoa simu za kisasa aina mbili – iPhone 6 na aina nyingine kubwa zaidi, iPhone 6 Plus.

Zote mbili ni kubwa kuliko toleo za mwanzo – huku skrini zikiwa na ukubwa wa sentimita 11.9 na 14.0.

Pia ni takriban nusu ya milimita kwa wembamba.

Imeimarisha muonekano wake kwa kile walichoita “retina HD”, ambapo itakuwa inapakua taarifa kwa kasi zaidi na kuahidi bateri kudumu kwa muda mrefu zaidi.

Apple ilishuhudia mauzo yake ya simu za kisasa kushuka duniani kutoka 13% hadi 11.7% kati ya mwaka 2013 mwishoni na mwaka 2014, kulingana na utafiti wa kampuni ya IDC.

Hata hivyo, mauzo ya Android yaliongezeka kutoka 79.6% hadi 84.7% katika kipindi hicho hicho cha Aprili hadi Juni, huku Samsung ikiwa na mauzo zaidi na kampuni ya Huawei na Lenovo za China ambazo zinaonekana kushamiri kwa kasi.

“Faida kubwa ya Apple ya kutengeneza skrini kubwa zaidi si kwamba inataka kuvutia watu wanunue simu zao, lakini kuzuia wateja wake kukimbia, hasa kukimbilia Samsung Galaxy Note,” alisema John Delany, mkuu wa timu ya Ulaya ya IDC.

“Liko wazi kuwa wateja wengi wa soko la Apple wanataka simu yenye ukubwa zaidi, alisema

Chanzo: BBC
 Imetafsiriwa na Mwandishi wetu









No comments:

Post a Comment