Thursday 2 April 2015

CHUO KIKUU KENYA CHASHAMBULIWA



Map showing Garissa in Kenya

Watu wenye silaha waliovaa barakoa wamevamia chuo kikuu kimoja karibu na mpaka wa Somalia kaskazini-mashariki mwa Kenya, wakiua watu wawili na kujeruhi takriban 30.

Majeshi yamezunguka chuo kikuu cha Garissa na kujaribu kupambana na washambuliaji.

Walioshuhudia walizungumzia watu hao wenye silaha wakifyatua risasi ovyo bila kujali ni nani na hivyo kuhofiwa kuwa idadi ya waliokufa inaweza kuongezeka.

Haiko wazi nani anahusika na shambulio hilo, lakini wapiganaji wa al-Shabab wamekuwa wakiishambulia Kenya mara kwa mara.

Garissa na maeneo mengine ya mpakani yamekuwa yakishambuliwa mara nyingi.

No comments:

Post a Comment