Kuna mtazamo tofauti sana kwa wanaume wanaowafuata machangudoa. Lakini wanajieleza vipi kuhusu kulipa kwasababu ya ngono?
Fred na Laura hufanya matembezi, wakati wa weekend hushinda pamoja, huenda sokoni pamoja na aghlabu hula chakula pamoja.
Watazungumza na kucheka kwa vitu walivyoona kwenye televisheni. Lakini pia hugombana.
Jikoni kwa Fred, wakati anaandaa chakula cha usiku, Laura hukaa na kuchekacheka, akikiri kuwa bora si yeye anapika.
Kama wapendanao wowote, wana siku za raha na za maudhi pia. Lakini hawa si wapendanao wa kawaida.
Fred anamlipa Laura ili ashinde naye, na kufanya naye ngono pia.
Wamekuwa katika mpango huo kwa miaka sita.
Mjadala
wa iwapo kuna tatizo kulipia ngono, na je ihalalishwe, bado ni motomoto
na hamna jibu kamili.
Pamoja na malumbano hayo, swali moja si kawaida
kuulizwa – kitu gani huwavuta wanaume kuwalipa wanawake kulala nao?
“Mara
ya kwanza tulikutana kwenye mtandao,” anasema Fred ambaye sasa
amestaafu, “na nikamwuuliza kama angependa kuwa nami hotelini usiku
mzima.”
Anasema ilikuwa kama wapenzi wakikutana mara ya kwanza, “tulitaka kujuana kwanza.”
“Sasahivi
tunajuana sana, yaani mno, kiasi ambacho Fred huingiza tu pesa kwenye
akaunti yangu kupitia mtandao kabla sijaenda kumwona,” anasema Laura.
Fred
anaishi kijijini na kwa miaka mingi amekuwa akimtunza mama yake.
Anasema hakupata nafasi ya kukutana na watu kwahiyo akaamua kulipia
ngono.
"Kusema ukweli haikuwa sana kuhusu ngono, zaidi ilikuwa
kuwa karibu tu na mwanamke, na kama hutoki ukajichanganya na watu basi
ni vigumu sana kufikiria utapataji hayo yote."
 |
| Baadhi hutaka tu kuwa karibu na mwanamke na wala si suala la ngono lenyewe |
- Robert amekuwa kwenye ndoa kwa miaka mingi.
“Niliishia
kuwa mwanamme ninayependa sana kufanya mapenzi ambaye nilioa mwanamke
ambaye havutiwi kabisa na hilo – au hata kukumbatiwa, kubusiana na
mengineyo.
"Ni mtu mwema, tena mwema sana. Kwa mambo mengine yote tunapatana sana, lakini si kitandani.”
Robert atadunduliza pesa chungu nzima ili tu aweze kulipia ngono.
“Nilitaka
kudumisha ndoa yangu,” anasema, “Nilitaka nifanye yote sahihi kwa mke
wangu, kwahiyo suluhu nilioiona ni kulipia ngono.”
Dhana ya kwamba
binadamu anaweza kuuzwa kimaadili bado inaleta utata. Wakati
machangudoa husema hawauzi miili yao, lakini kama wafanyakazi wengine,
wanauza vipaji na ujuzi wao. Wanasema uchangudoa usingekuwa uhalifu na
si jambo la kunyanyapaliwa, basi matatizo mengi yangetoweka.
Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu