Showing posts with label Makala. Show all posts
Showing posts with label Makala. Show all posts

Sunday 7 December 2014

ZARI 'THE BOSS LADY' ANAVYOWIKA TANZANIA

 
Wengi tunamfahamu kama Zari The bossy lady lakini jina lake halisi ni Zarinah Hassan mwanamuziki wa Uganda ambaye ameweka makazi yake nchini Afrika Kusini.

Licha ya kuwa kwenye tasnia ya burudani kwa muda mrefu, lakini umaarufu wake umeongezeka maradufu tangu alipoanza kuwa karibu na mwanamuziki Diamond Platinumz.

Ukaribu baina ya nyota hao umezua maswali mengi hasa baada ya kuzagaa kwa picha zao zinazowaonyesha wakiwa kwenye mapozi yenye utata.

Pamoja na kuwa wenyewe wamekanusha kuwa na uhusiano wa kimapenzi na kudai kuwa kuna kazi ya sanaa wanaifanya pamoja lakini vyombo vya habari vimekuwa vikiwamulika.

Kana kwamba hiyo haitoshi, siku za hivi karibuni mrembo huyu wa Uganda ameonyesha kuzidi kuwa karibu na Diamond katika shughuli mbalimbali ikiwemo kwenye hafla ya utoaji tuzo za muziki za Channel O zilizofanyika nchini Afika Kusini.

Monday 1 December 2014

MUHAMMAD: MAARUFU KWA WATOTO WA KIUME, UK



Muhammad limekuwa jina maarufu kwa watoto wa kiume nchini Uingereza, mtandao wa BabyCentre umedai.

Wakati huohuo majina ya kiarabu yamezidi kutumika zaidi.

Vipindi vya televisheni kama vile Game of Thrones pia vimechangia sana kutoa majina ya kizazi kijacho.

Orodha ya majina 100 bora ya watoto kwa mwaka 2014 imeonyesha Muhammad imepanda nafasi zaidi ya 27 kutoka mwaka jana hadi kufika namba moja.

Jina hilo limepata nafasi hiyo baada ya kuchaguliwa na watu 56,157 wa wanachama wa mtandao wa BabyCentre.co.uk waliojifungua mwaka 2014.

Kwa ujumla kumekuwa na ongezeko kubwa la majina ya kiarabu, huku Nur likiwa jipya kuingia katika orodha hiyo katika majina 100 bora ya kike, likiruka hadi nafasi ya 29, na Maryam likipanda mara 59 na kuchukua nafasi ya 35.

Omar, Ali na Ibrahim ni majina mapya kuingia katika 100 bora za kiume.

Sophia ndio namba moja katika majina ya watoto wa kike, na kupata umaarufu tena katika orodha ya mtandao wa BabyCentre nchini Marekani, Brazil, Hispania na Urusi mwaka jana.

Lakini jina linalotamba zaidi upande wa watoto wa kike ni Maryam, huku majina mapya zaidi ni Nur, Emilia na Gracie.

Chanzo: www.theguardian.com

NDOA YA WATU WENGI KWA MPIGO YAFUNGWA BRAZIL



Mass wedding in Rio de Janeiro

Takriban wapendanao 2,000 nchini Brazil wameoana katika eneo moja mjini Rio de Janeiro, kwenye harusi kubwa ya watu wengi kwa pamoja iliyoweka historia mjini humo.

Tukio hilo la kila mwaka, linalopigiwa chapuo na mamlaka za eneo hilo, lina nia ya kusaidia wapendanao wenye kipato kidogo wasio na uwezo wa kulipia gharama za harusi.


Mamlaka za Rio zilikodisha treni maalum kwa ajili ya wapendanao hao na wageni wao waalikwa.

Takriban watu 12,000 walihudhuria shughuli hiyo katika uwanja wa Maracanazinho.

Majaji walijitolea kuidhinisha shughuli hiyo.



Mass wedding in Rio de Janeiro
Watarajiwa wenye kipato cha dola 640 kwa mwezi waliruhusiwa kufungishwa ndoa kwenye shughuli hiyo 

Wapendanao hao pia walifungishwa ndoa iliyobarikiwa na askofu wa Kikatoliki na padri pia.

Tukio hilo limepewa jina la Dia do Sim", au "Siku ya Nakubali” yaani “I Do Day".

Wengi walioozeshwa walikuwa wakikaa pamoja kwa muda mrefu.

Bw Moraes amekuwa na Ana Rosangela Azevedo,mwenye umri wa miaka 31, tangu mwaka  2010 na mapema mwaka huu waliamua kuhalalisha mahusiano yao.

Saturday 29 November 2014

IDADI YA UTUMWA UINGEREZA 'KUBWA MNO'



Woman victim (posed by model)

Inawezekana kuwepo waathirika wa utumwa kati ya 10,000 hadi 13,000 Uingereza, idadi kubwa kuliko takwimu za awali, wizara ya mambo ya ndani imependekeza.

Waathirika wa utumwa wa kisasa ni pamoja na wanawake wanaolazimishwa kuingia kwenye biasahara ya uchangudoa, wafanyakazi wa ndani “wanaofungiwa”, na wanaofanya kazi mashambani, viwandani na kwenye boti za uvuvi.

Takwimu za mwaka 2013 ni mara ya kwanza kwa serikali hiyo kutoa idadi rasmi ya ukubwa wa tatizo hilo.

Wizara ya mambo ya ndani imeanzisha mkakati wa kupambana na utumwa huo.

Imesema waathirika hao inahusisha watu kutoka zaidi ya nchi 100 – na zaidi kutoka Albania, Nigeria, Vietnam na Romania – pamoja na watoto na watu wazima waliozaliwa Uingereza.

Mwaka jana Kituo cha Takwimu za Shirika la Uhalifu wa Taifa wa Kuuza Binadamu kilisema waathirika wa utumwa nchini Uingereza ilikuwa 2,744.

Tathhmini hiyo ilitolewa kwenye vyanzo mbalimbali ikiwemo polisi, idara ya uhamiaji, na mashirika ya kutoa misaada.

MALAWI NA TANZANIA BADO ZAZOZANIA ZIWA NYASA



Kile kilichoonekana kuanza kama mzaha kati ya Tanzania na Malawi kuhusu umiliki wa Ziwa Nyasa, sasa kimeanza kuchukua sura mpya kwa kila nchi kuendelea kutekeleza kitu inachokiamini kuwa ni sahihi.

Baada ya kutokea vuta nikuvute kati ya nchi hizo mbili zilizokuwa marafiki wa miaka mingi, marais wastaafu kutoka Msumbiji, Joaquim Chissano, Festus Mogae wa Bostwana na Thabo Mbeki wa Afrika Kusini walipewa jukumu la kutafuta maridhiano.

Hivi karibuni marais hao walikutana na Rais Peter Mutharika kwa ajili ya kuzungumzia jambo hilo, lakini kwa bahati mbaya walichodhani kuwa ni jambo dogo, kiligeuka kuwa ‘mfupa mgumu’ baada ya rais huyo kusema Tanzania haimiliki hata inchi moja ya Ziwa Nyasa.

Kama hiyo haitoshi, Mutharika anasema kuwa msimamo wake hauwezi kubadilika kwa kuwa mipaka ya nchi hizo mbili iliwekwa na wakoloni na kuipa uhalali Malawi umiliki wa ziwa hilo.

Wakati hayo yakiendelea huko Malawi, hapa nchini Serikali inaendelea na mipango ya kuboresha miundombinu ndani ya ziwa hilo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa meli yenye uwezo wa kubeba abiria 200 na mizigo tani 200.

Tuesday 25 November 2014

MAHAKAMANI KWA KUMFANYA BINTI KUWA 'MWEUPE'





 






















Halle Berry amempeleka aliyekuwa mpenzi wake Gabriel Aubry mahakamani kwa madai ya kutaka kubadilisha muonekano wa binti yao ili awe mweupe.

Anadai Aubry amezinyoosha nywele za Nahla zilizojinyonganyonga na kuzipaka rangi kwa nia ya kumfanya asionekane Mmarekani mweusi.

Nyaraka za mahakamani zinamshutumu Aubry kwa kumsababishia “uharibifu wa kisaikolojia na wa mwili” kwa binti yao mwenye umri wa miaka sita na kumsababishia aanze kuwaza “kwanini muonekano wake wa asili hautoshi ”.

 “Nataka mimi na Gabriel tuchukue uamuzi pamoja juu ya binti yetu, ukuaji wake, maendeleo yake na maisha yake kwa ujumla,” alisema Berry kwenye nyaraka hizo.

Wakili wa Berry, Steve Kolodny, ndie aliyekuwepo mahakamani siku ya Jumatatu pamoja na Aubry.
Jaji alitoa uamuzi kuwa hakuna mzazi hata mmoja anayeweza kubadili muonekano wa Nahla kutoka asili yake.

Wapenzi hao waliachana mwaka 2010 baada ya kuwa pamoja kwa miaka minne.


Chanzo: www.independent.co.uk
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu