Saturday 29 November 2014

IDADI YA UTUMWA UINGEREZA 'KUBWA MNO'



Woman victim (posed by model)

Inawezekana kuwepo waathirika wa utumwa kati ya 10,000 hadi 13,000 Uingereza, idadi kubwa kuliko takwimu za awali, wizara ya mambo ya ndani imependekeza.

Waathirika wa utumwa wa kisasa ni pamoja na wanawake wanaolazimishwa kuingia kwenye biasahara ya uchangudoa, wafanyakazi wa ndani “wanaofungiwa”, na wanaofanya kazi mashambani, viwandani na kwenye boti za uvuvi.

Takwimu za mwaka 2013 ni mara ya kwanza kwa serikali hiyo kutoa idadi rasmi ya ukubwa wa tatizo hilo.

Wizara ya mambo ya ndani imeanzisha mkakati wa kupambana na utumwa huo.

Imesema waathirika hao inahusisha watu kutoka zaidi ya nchi 100 – na zaidi kutoka Albania, Nigeria, Vietnam na Romania – pamoja na watoto na watu wazima waliozaliwa Uingereza.

Mwaka jana Kituo cha Takwimu za Shirika la Uhalifu wa Taifa wa Kuuza Binadamu kilisema waathirika wa utumwa nchini Uingereza ilikuwa 2,744.

Tathhmini hiyo ilitolewa kwenye vyanzo mbalimbali ikiwemo polisi, idara ya uhamiaji, na mashirika ya kutoa misaada.

No comments:

Post a Comment