Saturday 8 November 2014

WILLIAMS HAKUWA AMETUMIA DAWA ZA KULEVYA



Williams with wife Susan Schneider
Mke wake Susan Schneider ameomba Williams akumbukwe kwa furaha aliyoleta duniani
Robin Williams hakuwa akitumia dawa za kulevya au pombe katika muda aliojiua, mamlaka za California zimesema.

Muigizaji huyo, mwenye umri wa miaka 63, alikutwa nyumbani kwake California Agosti 11 kwa kile ambacho baadae mamlaka husika zilisema alijiua.

Ripoti iliyotolewa na afisa aliyekuwa akichunguza kifo chake siku ya Ijumaa kiligundua kuwa Williams alikufa kwa kukosa pumzi kutokana na kujinyonga.

Williams, aliyepata umaarufu kutokana na uigizaji wake katika filamu kama Mrs Doubtfire na Good Will Hunting, alikuwa akipata matibabu kutokana na maradhi ya msongo wa mawazo.

Mtoa burudani huyo alionekana mara ya mwisho akiwa hai na mke wake Agosti 10, na kukutwa kafariki dunia siku ya pili yake.

Siku mwili wake ulipokutwa, ni msaidizi wake aliamua kufungua mlango baada ya kuona kimya kila alipougonga, mamlaka zimesema.

Msaidizi wake huyo aliingia chumbani na kumkuta Williams akiwa ameshafariki dunia.

 Williams alishinda tuzo ya Academy katika nafasi aliyoigiza kwenye filamu ya Good Will Hunting na pia alikuwa muigizaji mkuu katika filamu kama vile Good Morning Vietnam na Jumanji.


No comments:

Post a Comment