Tuesday 4 November 2014

SERIKALI YAKATA RUFAA KESI YA PISTORIUS



Oscar Pistorius pictured on 17 October 2014

Waendesha mashtaka wa serikali nchini Afrika Kusini wamekata rufaa dhidi ya mashtaka na hukumu aliopewa mwanariadha Oscar Pistorius.

Katika nyaraka za rufaa hiyo, waendesha mashtaka wamesema hukumu hiyo inawashangaza kutokana na kuwa nyepesi, isiyofaa na isingeweza kutolewa na mahakama yoyote makini.

Mwezi uliopita, Pistorius alianza kutumikia kifungo cha miaka mitano kwa mauaji ya kukusudia au kutokukusudia (culpable homicide) ya mpenzi wake, Reeva Steenkamp.

Alifutiwa mashtaka ya mauaji ya mpenzi wake huyo.

Pistorius anaruhusiwa kuomba kutumikia kifungo cha nyumbani kwa muda utakaobaki baada ya kukaa gerezani kwa miezi kumi.

Chanzo: AP, AFP


No comments:

Post a Comment