Tuesday 4 November 2014

VIFIJO NA VIGELEGELE : NYANI WAOANA INDIA



Monkey wedding in Bihar

Zaidi wa wanakijiji 200 kaskazini mwa India wamehudhuria sherehe ya harusi ya nyani wawili.

Harusi hiyo iliandaliwa na mmiliki wa nyani hao, ambaye alisema nyani wa kiume alikuwa “kama mtoto wake wa kuasili”.

Sherehe hiyo ilifanyika siku ya Jumatatu katika wilaya ya Bettiah kwenye jimbo la Bihar, huku “biharusi” akiwa amevaa gauni la rangi ya machungwa na “bwana harusi” kavaa fulana ya njano.

Nyani huyo wa kiume mwenye umri wa miaka 13 aitwaye Ramu, na bi harusi wake, nyani wa kike akiitwa Ramdulari, walipandishwa juu ya SUV lililojazwa maua huku pakiwepo mziki.

Mamia ya wanakijiji walisema mtaani kuwashuhudia “wanandoa” hao.

Udesh Mahto, mfanyakazi wa kawaida aliye na watoto wa kiume watatu, alisema Ramu alikuwa “kama mtoto wake mkubwa”.

"Nilitaka kumwozesha yeye mwanzo,"alisema.

Bw Mahto alimleta Ramu kutoka Nepal kama miaka saba iliyopita, na baadae kumnunua Ramdulari kutoka kijiji kengine.

"Mwanzoni walikuwa hawapatani. Lakini baadae wakaanza kupendana, kwahiyo nikaamua kuwaozesha, “ alisema.


No comments:

Post a Comment