Friday 7 November 2014

UBISHANI: NANI HASA ALIYEMWUUA BIN LADEN?



Retired US Navy Seal Robert O'Neill (file image)
Robert O'Neil anasema yeye ndiye aliyempiga risasiOsama bin Laden  kichwani

Mabishano ya umma yameibuka ya komandoo yupi wa Marekani aliyefyatua risasi iliyomwuua Osama bin Laden, zaidi ya miaka mitatu baada ya kifo cha kiongozi huyo wa al-Qaeda.

Aliyekuwa mwanajeshi wa nchi hiyo Seal Robert O'Neill, mwenye umri wa miaka 38, ameliambia gazeti la the Washington Post katika mahojiano kuwa yeye ndiye aliyefyatua risasi hiyo.

Kauli yake inapingana na ya Matt Bissonnette, mwanajeshi mwengine aliyehusika katika uvamizi, kwenye kitabu chake alichochapisha mwaka 2012.

Kiongozi huyo wa al-Qaeda aliuawa kwenye uvamizi uliofanywa na wanajeshi wa Marekani katika eneo alilokuwa akiishi huko Abbottabad, Pakistan.

Osama bin-Laden addresses a news conference in Afghanistan in this May 26, 1998 file photo.
Osama bin Laden
Aghlabu wanajeshi hao (Navy Seals) hutii sheria ya ukimya linalowakataza kupata sifa yoyote kutoka kwa umma kutokana na hatua walizochukua.

Bw O'Neill, aliyestaafu mwaka 2012, awali alielezea habari yake bila kuonekana sura kwenye jarida la Esquire.

Ilitakiwa ajitambulishe hadharani kwenye mahojiano ya televisheni baadae mwezi huu, lakini taarifa za mahojiano hayo yaliwakasirisha waliokuwa wanajeshi wakati huo.

Bw O'Neill alisema yeye na mwenzake mwengine – ambaye utambulisho wake unabaki kuwa siri – walipanda ngazi mpaka ghorofa ya tatu ya makazi yake Abbottabad, Pakistan, na kumwona Bin Laden akichungulia nje ya mlango mojawapo ya vyumba vya nyumba hiyo.

No comments:

Post a Comment