Monday 17 November 2014

POLIS WAVAMIA MISIKITI MOMBASA, KENYA


 File photo: A police officer hits men as police storm the Masjid Musa Mosque and detain alleged jihadist radicals in the Majengo area of Mombasa, 2 February 2014
Polisi wa Kenya wamempiga risasi na kumwuua mtu mmoja na kuwakamata zaidi ya wengine 250 katika uvamizi walioufanya kwenye misikiti miwili mjini Mombasa.

Polisi wanasema misikiti hiyo imetumika kuajiri wafuasi wa kundi la Kisomali, al.-Shabaab, ambalo limefanya mashambulio kadhaa Kenya.

Wamesema  msikiti Musa na  Shakinah  zilikuwa zikitumika kuhifadhi silaha.

Magurunedi, visu na bendera ya al-Shabab vinadaiwa kukamwatwa wakati wa uvamizi huo.

Tishio za ghasia zimechangia sana kuyumbisha sekta ya utalii hasa upande wa pwani ya Kenya.



No comments:

Post a Comment