Monday 3 November 2014

MJUMBE WA MALAWI 'AMPUUZA' BW MUGABE



Thoko Banda
Thoko Banda amesema hatopuuza wajibu wake wa kutetea haki za bindamu kwasababu ya kazi

Mwanadiplomasia wa Malawi amekataa kazi ya kuwa balozi nchini Zimbabwe kwasababu anapinga udikteta, ameiambia BBC.

"Watu wenye hisia wanatakiwa kuwaunga mkono watu wa Zimbabwe, hasa wale wanaoishi katika hali ya umaskini," alisema Thoko Banda.

Mwaka 2006, iliripotiwa kuwa alimwita Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe "mjinga".

Bw Banda aliiambia BBC hatotumia maneno hayo tena.

Bw Mugabe amekuwa madarakani Zimbabwe tangu mwaka 1980 lakini amekana kukikuka haki za binadamu.

Serikali zote mbili hazijasema lolote kuhusu kauli hiyo ya Bw Banda.

Bw Mugabe anabaki kuwa kiongozi mwenye ushawishi mkubwa barani Afrika na anaungwa mkono na viongozi wengi wa bara hilo, licha ya kukosolewa sana na nchi za kimagharibi.


No comments:

Post a Comment