Tuesday 11 November 2014

KAPTENI WA KOREA KUSINI MIAKA 36 JELA



Sewol ferry captain Lee Joon-Seok (C) is escorted upon his arrival at the Gwangju District Court in the south-western South Korean city of Gwangju

Kapteni wa kivuko cha Korea kusini kilichozama mwezi Aprili amekutwa na kosa la kudharau na kuhukumiwa miaka 36 jela.

Kivuko hicho kilikuwa na abiria 476 kilipozama. Zaidi ya 300 wamefariki dunia, wengi wao wakiwa wanafunzi.

Lee Joon-seok ni miongoni mwa wafanyakazi 15 wa kivuko hicho walioshtakiwa kutokana na tukio hilo, miongoni mwa balaa kubwa kutokea majini Korea kusini.

Waendesha mashtaka wamemshatki kwa mauaji ‘homicide’ na kutaka  apewe adhabu ya kifo, lakini majaji walimfutia hukumu hiyo.

Lee ana zaidi ya umri wa miaka 60, na alikubali mahakamani kuwa katika siku zake zilizobaki duniani abaki gerezani.

Majaji walisema bila shaka si yeye peke yake anayehusika na tukio hilo na wamekubali kuwa kudharau kwake hakumaanishi alikuwa na nia ya kuua.

No comments:

Post a Comment