Tuesday 4 November 2014

WANAWAKE 'RUKHSA' KUPAKA WAIGIZAJI VIPODOZI



A make-up studio in Delhi

Mahakama Kuu ya India imesema hatua ya kuzuia wanawake wenye fani ya kupaka watu vipodozi (make-up artist) kwa miaka 59 katika uwanda wa filamu wa nchi hiyo ni kinyume cha sheria na lazima iondolewe.

Majaji wawili wamesema ubaguzi wa kijinsia ni kukiuka sheria za katiba.

Chama kimoja cha wafanyakazi chenye ushawishi mkubwa nchini humo miaka mingi kimekuwa kikisema wanaume wanahitaji ajira.

Wanawake wanaruhusiwa kufanya kazi kama wanamitindo wa nywele katika utengenezaji wa filamu lakini yeyote atakayejaribu kumpaka muigzaji kipodozi hutishiwa au hata kudhalilishwa.

"Ubaguzi huu utaendelea vipi? Hatuwezi kukubali. Haiwezi kuruhusiwa chini ya katiba yetu. Kwanini mwanamme tu aruhusiwe kupaka watu vipodozi? Alinukuliwa akisema jaji Dipak Misra na UU Lalit katika gazeti la India Express.

“Hatuoni sababu kwanini mwanamke azuiwe kutia watu vipodozi ilimradi ana sifa zinazostahili."


No comments:

Post a Comment