Sunday 30 November 2014

AJERUHIWA KWA CHOO CHA KUIBUKA ARDHINI



A scooter lies in pieces after a public toilet suddenly emerged from the ground

Mtu mmoja katika mji wa Amsterdam amejeruhiwa baada ya choo cha umma kinachomazishwa ardhini kuibuka ghafla  bila kutarajia.

Mtu huyo alijeruhiwa na mfano wa motokari iliyoruka angani kwa inayoitwa choo cha Urilift kilichoibuka ghafla.

Kwa sasa anapatiwa matibabu hospitalini kwa majeraha madogo.

Vyoo hivyo vimezagaa maeneo mengi katikati ya Amsterdam, na huibuka kutoka ardhini usiku kuzuia watu kukojoa mitaani.

Walioshuhudia waliripoti kusikia mlio mkubwa sana wakati wa ajali hiyo.

Mtu mmoja aliweka picha baada ya tukio hilo katika mtandao wa kijamii wa twitter na kuandika : “Nimepita pembezoni mwa mlipuko kama dakika mbili zilizopita. Nahisi nina bahati.”

Haiko wazi nini kilisababisha tukio hilo.

Matokeo ya uchunguzi huo yanatarajiwa kutolewa mwishoni mwa juma.


Vyoo vya Urilift hupatikana Amsterdam na katika nchi mbalimbali barani Ulaya.


Chanzo: Independent.co.uk

No comments:

Post a Comment