Tuesday 4 November 2014

MGONGANO WA KISIASA ZAMBIA



Egar Lungu
Edgar Lungu ni kiungo muhimu kwenye chama cha Patriotic Front

Waziri wa ulinzi wa Zambia ambaye ana ndoto za kuwania urais, Edgar Lungu amerejeshwa kwenye nafasi yake ya ukatibu mkuu wa chama tawala, baada ya kufukuzwa siku ya Jumatatu na rais wa mpito Guy Scott.

Waandishi wanasema kumekuwa na mvutano wa madaraka unaochipuka wa nani atakayemrithi aliyekuwa rais Michael Sata, aliyeaga dunia wiki iliyopita.

Katika taarifa, iliyotiwa saini na wote wawili Bw Scott na Bw Lungu, chama tawala, the Patriotic Front, kilisistiza umuhimu wa umoja huku Zambia ikiomboleza kifo cha kiongozi huyo.

Usiku wa Jumatatu, polisi walirusha mabomu ya machozi kusambaza wafuasi wa Bw Lungu waliokasirishwa na kufurumushwa kwake.

No comments:

Post a Comment