Saturday 15 November 2014

HAKUNA TENA EBOLA DRC



 A training session for Congolese health workers to deal with Ebola virus in Kinshasa, Democratic Republic of Congo on 21 October 2014

Mlipuko wa miezi mitatu wa Ebola huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo umeisha baada ya kusababisha vifo vya watu 49, waziri wa afya wa  nchi hiyo alisema.

Felix Kabange alisema hakuna wagonjwa wapya waliosajiliwa tangu tarehe 4 Oktoba.

Mlipuko huo nchini humo hauhusiani kabisa na ule wa Afrika magharibi uliosababisha vifo vya zaidi ya watu 5,000.

Ebola kwa mara ya kwanza uligunduliwa mwaka 1976 karibu na Ebola River ambapo sasa ndio Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo

Tangazo hilo la Jumamosi limetolewa baada ya mtu wa mwisho kupata ugonjwa huo nchini humo siku 42 zilizopita.

No comments:

Post a Comment