Saturday 29 November 2014

MUBARAK WA MISRI AFUTIWA MASHTAKA YA MAUAJI



 Hosni Mubarak in court in Cairo, 29 November

Mahakama mjini Cairo imemfutia mashtaka aliyekuwa rais wa Misri Hosni Mubarak kwa jaribio la kupanga kuwaua waandamanaji wakati wa ghasia za kumpindua mwaka 2011.

Mahakama uliibuka kwa shangwe baada ya jaji kuhitimisha kesi ya Mubarak kwa kufuta mashtaka yaliyohusishwa na mauaji ya mamia ya watu.

Pia alifutiwa mashtaka ya ufisadi iliyohusisha mauzo ya gesi Israel.

Mubarak, mwenye umri wa miaka 86, anatumikia kifungo kingine cha miaka mitatu kwa ubadhirifu wa mali ya umma.

No comments:

Post a Comment