Friday 28 November 2014

MALEMA ASIMAMISHWA BUNGENI, AFRIKA KUSINI


 Julius Malema speaks as he launches his Economic Freedom Fighters party in Johannesburg, South Africa on 11 July 2013

Mkuu wa chama cha upinzani cha Afrika kusini Julius Malema na wabunge wake 11 wamesimamishwa katika bunge bila malipo baada ya kumdhalilisha rais wa nchi hiyo.

Wakati Rais Jacob Zuma alipolihutubia bunge mwezi Agosti, wanachama wa Economic Freedom Fighters (EFF) walipiga kelele wakisema "lipa pesa zetu".

Walikuwa wakimaanisha matumizi ya dola milioni 23 ya pesa za serikali kukarabati nyumba yake binafsi huko Nkandla.

Mapema mwezi huu, bunge lilimfutia makosa.

Chama hicho cha EFF kilisema kitapambana mahakamani kusimamishwa huko, ambapo ni kati ya siku 14 hadi 30.

No comments:

Post a Comment