Thursday 6 November 2014

BURKINA FASO WAKUBALIANA SERIKALI YA MPITO



 Interim leader Lt Col Isaac Zida. Photo: 5 November 2014

Vyama vya kisiasa vya Burkina Faso vimekubali kuwa hatua ya mpito ya kisiasa nchini humo idumu kwa mwaka mmoja, ikifuatiwa na uchaguzi Novemba 2015.

Lakini mazungumzo kwenye mji mkuu Ouagadougou yalimalizika bila kuwa na makubaliano ya nani atakuwa kiongozi wa serikali ya mpito.

Jeshi limekuwa likishika hatamu tangu Rais Blaise Compaore alipolazimishwa kuachia madaraka wiki iliyopita baada ya maandamano mazito.

Umoja wa Afrika (AU) siku ya Jumatatu umeipa jeshi wiki mbili kukabidhi uongozi kwa raia au wkabiliane na vikwazo.

Lt Col Isaac Zida – kiongozi wa mpito anayeungwa mkono na jeshi baadae alikubali kufuata makataa (deadline) hayo.

Alikuwa wa pili katika makamanda waliokuwa wakimlinda rais.


No comments:

Post a Comment