Sunday 9 November 2014

WATOTO WA NCHI ZINAZOENDELEA WANA 'RAHA' ZAIDI




Unhappy child 

Watoto wa nchi zinazoendelea wana furaha zaidi na ni wenye kuridhika kuliko watoto wa Uingereza, utafiti mpya umeonyesha.

Ripoti ya The Children's Society's Good Childhood imeipa nafasi ya chini kuliko hata Romania, Brazil na Afrika kusini.

Ni ya tisa kati ya 11 zilizofanyiwa utafiti – kabla ya Korea kusini na Uganda- jinsi watoto walivyo na furaha na maisha yao.

Ripoti hiyo, iliyoangazia utafiti wa watoto 16,000 kutoka nchi hizo, imeonya hali duni ya maisha yao inaweza kuharibu afya ya watoto, elimu na maisha ya familia zao.

Takwimu zaidi kwenye utafiti huo pia zimependekeza kuwa Uingereza kote, nusu milioni ya watoto walikuwa na hali duni ya maisha.

Mkurugenzi mkuu wa Children's Society, Matthew Reed alisema wakati utoto ulikuwa una mwelekeo mzuri “kwa wengi” Uingereza, hali ya kwamba wengi hawakuwa na raha au kutoridhika na maisha yao isipuuzwe.

"Ripoti hii mpya inaonyesha wazi tuko nyuma ya nchi nyingi, zikiwemo nchi zinazoendelea, " Bw Reed alisema.

Kulingana na takwimu ambazo England ilikuwa ikilinganishwa nazo nyingine 10, mtoto mmoja wa Kiingereza kati ya wanane hakuwa na raha na umbile lake.

Ni watoto wa Korea kusini tu miongoni mwa nchi hizo nao walikuwa wana watoto ambao hawakuridhika na maumbo yao.

'Sikiliza kwa makini'         

Watoto England walikuwa wana hisia chanya kuhusu marafiki, nyumbani, pesa na mali, wakiwa nafasi ya sita miongoni mwa nchi 11.

Ripoti hiyo imegundua kuwepo uhusiano baina ya hali halisi ya mtoto na uwezo wa kiuchumi.

Takriban theluthi ya watoto walisema familia zao zimeathirika “kwa kiwango cha kutosha” au “kiwango kikubwa” na msukosuko wa fedha.

Ilisema watoto wanaojihisi maskini wangetarajiwa maradufu kusema kuwa hawana furaha na mara tatu zaidi wangesema wana maisha duni.

"Watoto wanatuambia kuwa hawana raha kuhusu maisha yao ya usoni na maumbile yao, na pia mambo yanayowapa furaha zaidi ni kama kushirikishwa katika shughuli mbalimbali, kuwa na urafiki imara na uwezo wa kuingia kwenye mitandao,” Bw Reed aliongeza.

"Ni muhimu sana kwa sote – kuanzia watunga sera mpaka wazazi na walimu – kuwasikiliza kwa makini wanachotaka kutuambia.”

Nchi 11 zilizofanyiwa utafiti katika ripoti hiyo ni England, Romania, Uhispania, Israel, Brazil, Marekani, Algeria, Afrika kusini, Chile, Korea kusini na Uganda.

Takriban watoto 16,000 walifanyiwa utafiti - 3,000 kutoka England na kutoka darasa la nne, sita na nane.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu


      

No comments:

Post a Comment