Friday 7 November 2014

EBOLA YAPUNGUA LIBERIA



 A Liberian woman prays for the end of Ebola in Monrovia, Liberia - 31 October 2014

Liberia imeshuhudia punguzo kubwa la idadi ya wagonjwa wapya walioambukizwa Ebola, shirika la madaktari wasiokuwa na mipaka Medecins Sans Frontieres (MSF) limethibitisha.

Limesema moja ya vituo vyake vinavyotoa matibabu Liberia haina wagonjwa wowote kwa sasa – lakini likaonya bado maambukizi ya Ebola yanaongezeka Guinea na Sierra Leone.

MSF, linaloajiri maelfu ya wafanyakazi Afrika magharibi, linaonekana kuwa shirika bora lenye taarifa sahihi za Ebola.

 Takriban wagonjwa 5,000 kati ya 14,000 wamekufa kutokana na virusi vya ugonjwa huo.

Chris Stokes, Mkuu wa MSF wa masuala ya Ebola, ameiambia BBC kwamba kupungua kwa idadi ya watu walioathirika na virusi vya ugonjwa huo kumetoa fursa kwa wafanyakazi wa afya kuongeza jitihada.

Lakini alisema ugonjwa huo unaweza “kuibuka” tena, akisema Guinea imeanza kuwa na ongezeko la wagonjwa hao tena licha ya maambukizi kutangazwa kudhibitiwa mara mbili.

Ili kudhibiti ugonjwa huo, Bw Stokes aliongeza, inatakiwa idhibitiwe Liberia, Guinea na Sierra Leone kwa mara moja.

No comments:

Post a Comment