Tuesday 25 November 2014

'MILIPUKO MIWILI' MJINI MAIDUGURI, NIGERIA


 Boko Haram leader Abubakar Shekau with fighters. 31 Oct 2014


Wanawake wawili wa kujitoa mhanga wamejilipua kwa mabomu katika soko lenye mkusanyiko wa watu wengi katika mji wa Maiduguri kaskazini mwa Nigeria na kusababisha vifo vingi, walioshuhudia walisema.

Takriban watu 30 waliuawa baada ya  vijana hao wawili walipojilipua, walioshuhudia waliwaambia shirika la habari la AP.

Mmoja aliyeshuhudia Sani Adamau aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa mlipuko wa pili ulitokea watu walipokuwa  wanajaribu kuwasaidia wale waliojeruhiwa kwenye mlipuko wa kwanza.

Kundi la wapiganaji la Boko Haram limeshafanya mashambulio mengi Nigeria.

Kundi hilo lilianzia Maiduguri, mji mkuu wa jimbo la Borno, baada ya kuundwa mwaka 2002, lakini tangu wakati huo limefurumushwa mjini humo na jeshi pamoja na makundi ya sungusungu.

Sasahivi linadhibiti maeneo makubwa ya miji na vijiji huko Borno, huku kukiwa na hofu ya kuiteka Maiduguri.

Boko Haram halijasema lolote kuhusu shambulio hili.



No comments:

Post a Comment