Sunday 23 November 2014

UCHAGUZI WA KWANZA TUNISIA BAADA YA MAGEUZI



Activists in Monastir, Tunisia. Photo: 2 November 2014

Raia wa Tunisia wanapiga kura katika uchaguzi wa kwanza wa Rais tangu “vuguvugu la mageuzi ya nchi za Kiarabu” kutokea mwaka 2011 na kuchochea mageuzi hadi nchi nyingine eneo hilo.

Zaidi ya watu 25 wanagombea kinyang’anyiro hicho, lakini aliye madarakani kwa sasa  Moncef Marzouki na Beji Caid Essebsi wanaonekana kukubalika zaidi.

Uchaguzi huo ni sehemu ya mpito wa kisiasa baada ya kupinduliwa kwa Zine al-Abidine Ben Ali.

Uchaguzi wa wabunge ulifanyika mwezi Oktoba.

Tunisia – nchi inayoonekana kiini cha mageuzi katika nchi za Kiarabu – pia inachukuliwa kuwa nchi iliyofanikiwa zaidi baada ya mageuzi hayo, na yenye ghasia kidogo kulingana na nchi nyingine.

No comments:

Post a Comment