Sunday 23 November 2014

KENYA YAUA 'WAPIGANAJI 100 WA ALSHABAB'



A Kenyan soldier patrols the scene of an attack on a bus, some 30km from Mandera town, in northern Kenya - 22 November 2014

Jeshi la Kenya limeua zaidi ya wapiganaji 100 wa al-Shabab waliohusishwa na shambulio baya sana kwenye basi, naibu rais wa Kenya alisema.

William Ruto alisema majeshi yamefanya misako miwili nchini Somalia, kuharibu vifaa na kambi ambapo shambulio hilo la basi lilipopangwa.

Katika shambulio la Jumamosi, wapiganaji waliwachomoa abiria wasio waislamu kutoka kwenye basi kaskazini mwa Kenya, na kuua 28.

Al-Shabab limefanya mfululizo wa mashambulio nchini Kenya tangu mwaka 2011, mwaka ambao Kenya ilipeleka majeshi Somalia kusaidia kupambana na wapiganaji.

Chanzo: BBC                            
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment