Saturday 22 November 2014

MASANDUKU YENYE 'KELELE' YAPIGWA MARUFUKU



Grand Canal, Venice, 27 Sep 2014
Venice, mji wenye mvuto mkwabwa wa watalii  nchini Italia

Mji wa Venice unafikiria kupiga marufuku utumiaji wa masanduku yanayotumia matairi yanayopiga kelele kwa madai yanawafanya watu kuwa macho usiku mzima.

Maafisa wanataka wageni wote kuachana na masanduku hayo au kutumia “yasiokuwa na makelele”  na mbadala uwe matairi yaliyojaa hewa au kimiminika.

Matumani ni kuwa hatua hiyo italinda pia mitaa ya kale ya mji huo.

Venice ni miongoni mwa miji mikubwa inayopata watalii wengi Italia, huku watu milioni 27 wakimiminika kila mwaka.

"Amri hiyo inatolewa kukabiliana na malalamiko mengi kutoka kwa raia mbalimbali katika miaka ya hivi karibuni kwa manispaa husika kuhusu kero kubwa inayosababishwa na watu kusogeza vitu mchana na usiku," kulingana na mtandao wa manispaa ya Venice.

Lakini meneja mmoja wa hoteli aliiambia BBC anahisi amri hiyo haitotekelezeka.

Alisema kama maeneo wanaotumia wapita njia ‘pavements’ yana makelele sana, basi mji huo ubadilishe seheumu hizo badala ya masanduku.

No comments:

Post a Comment