Friday 14 November 2014

WABUNGE NA POLISI WAPURUKUSHANA BUNGENI


 Police officers closing parliament's doors in Cape Town, South Africa in August 2014

Polisi wa kuzuia ghasia Afrika kusini wamepambana na wabunge wa upinzani saa chache baada ya bunge kumfutia rais Jacob Zuma tuhuma za matumizi ya dola milioni 23 za fedha za taifa kukarabati nyumba yake binafsi huko Nkandla.
Waliingilia kati baada ya mbunge wa upinzani Ngwanamakwetle Mashabela kurudia mara kwa mara kumwita Bw Zuma mwizi.
Wabunge wanne walijeruhiwa katika tafrani hiyo iliyotokea katika kikao cha usiku.
Mwezi Machi, mchunguzi wa ufisadi nchini humo alisema Bw Zuma ‘alifaidika kupita kiasi’ kutokana na ukarabati huo.
Mwendesha mashtaka Thuli Madonsela pia alimshutumu kwa kukiuka maadili na kupendekeza alipe fedha zilizotumika kukarabati vitu visivyohusiana na masuala ya usalama huko Nkandla, kwenye jimbo la KwaZulu Natal, lililo na bwawa la kuogelea na mabanda ya mifugo.


Jacob Zuma's Nkandla residence
Nyumba yake binafsi ina bwawa la kuogelea na mabanda kadhaa ya mifugo
Lakini ripoti ya kamati ya bunge – iliyopitishwa na wabunge walio wengi kutoka chama cha African National Congress (ANC) siku ya alhamis- imemsafisha Bw Zuma kuwa na kosa lolote.
Serikali nayo pia ilisema ilibidi fedha hizo kutumika kwa minajil ya usalama.
 

No comments:

Post a Comment