Monday 10 November 2014

WANAFUNZI WA SEKONDARI WAUAWA NIGERIA



Two children are treated at the general hospital in Potiskum, Nigeria on 10 November 2014
Wazazi wa watoto waliojeruhiwa wamekusanyika katika hospitali ya Potiskum

Takriban wanafunzi 46 wameuawa na mtu mmoja aliyejitoa mhanga, wanafunzi hao walipokuwa kwenye mstari shuleni kwenye mji ulio kaskazini-mashariki mwa Nigeria uitwao Potiskum, polisi walisema.

Polisi wanapendekeza kuwa Boko Haram ndio waliofanya shambulio hilo.

Gavana wa jimbo la Yobo amefunga shule zote za umma huko Potiskum na kuikosoa serikali kwa kutotatua tatizo hilo.

Tarehe 17 Oktoba serikali ya Nigeria ilidai imekubaliana na Boko Haram kusitisha mapigano.

Lakini wiki mbili baadae kiongozi wa kundi hilo, Abubakar Shekau alikana madai hayo na kusema kwenye video: “ Hatujasitisha mapigano na mtu yeyote. Hatujakubaliana na mtu yeyote. Ni uongo.”

1 comment: