
Ushiriki wa wanawake zaidi katika siasa na kazi nyingine
imepunguza idadi ya utofauti wa kijinsia duniani katika kipindi cha miaka 10
iliyopita, Jukwaa la Kiuchumi Duniani (WEF) limesema.
Utafiti wa mwaka wa jinsia wa WEF umethibitisha “mabadiliko makubwa” katika
nchi nyingi, huku nchi 105 zikiwa na usawa tangu mwaka 2005, mwandishi wa
ripoti hiyo amesema.
Iceland ndio inaongoza kwa miaka sita mfululizo, huku Yemen ikishikilia mkia.
WEF imeangazia zaidi uchumi, afya, elimu na ushiriki wa kisiasa katika nchi
142.
Mataifa sita tu - Sri Lanka, Mali, Croatia, Macedonia, Jordan na Tunisia – yameshuhudia
usawa wa kijinsia kuongezeka kwa ujumla tangu mwaka 2005, kulingana na WEF.
Moja ya sababu za mafanikio ya Iceland ni idadi ndogo ya watu nchini humo
wakati Yemeni ina idadi kubwa ya vifo na watoto wengi wa kike wenye umri wa
miaka sita hadi 14 hawajawahi kuhudhuria shule
Rwanda yafanya vyema
Mataifa ya Nordic yanaongoza, huku Finland, Norway na Sweden yanaifuata
Iceland katika tano bora.
Uingereza imeshuka kwa nafasi nane duniani na kufikia nafasi ya 26.
Rwanda imeingia katika orodha hiyo kwa mara ya kwanza na kuchukua nafasi ya
saba, na kuifanya nchi yenye mafanikio makubwa kiuchumi barani Afrika.
Mwandishi wa ripoti hiyo Saadia Zahidi alisema mafanikio ya Rwanda ni
kwasababu kuna karibu idadi sawa ya wanawake na wanaume wenye ajira – na katika
ofisi za wizara – na badala yake huduma za afya na elimu zimeimarika.
Mabadiliko ya mapato ya wanawake ndio iliyoiporomosha Uingereza, ilisema
WEF.
Msukosuko wa uchumi ndio umesababisha utofauti wa kipato wa kijinsia
kuongezeka Uingereza.
Kutaka kujua zaidi na kujua nchi yako iko nafasi ya ngapi, Bonyeza hapa
http://www.bbc.co.uk/news/world-29722848