Showing posts with label Siasa. Show all posts
Showing posts with label Siasa. Show all posts

Tuesday 10 March 2015

MPINZANI WA BURUNDI ALITOKA GEREZANI 'KIULAINI'


Hussein Radjabu during his trial in April 2008
Hussein Radjabu
Mpinzani mkuu nchini Burundi Hussein Radjabu ameiambia BBC kuwa alitoroka kutoka gerezani wiki iliyopita kwa kutembea “bila wasiwasi wowote”.

Polisi wa Burundi walisema maafisa wa gerezani walimsaidia kutoroka.

Radjabu alisema sasa yupo na wafuasi wake – lakini hakueleza ni wapi hasa alipo.

Aliyekuwa mkuu wa chama hicho tawala alikuwa akionekana mwenye ushawishi mkubwa mno nchini Burundi mpaka alipokamatwa mwaka 2007, baada ya kuwepo na tetesi za kutoelewana na Rais Pierre Nkurunziza.

Pierre Nkurunziza

Aliphojiwa na BBC, Radjabu alimtuhumu rais kwa kupanga kufukuzwa kwake chamani, pamoja na kumwuundia kesi ya njama ya kupindua serikali.

Radjabu ametoroka baada ya kutumikia miaka minane kati ya 13 ya hukumu yake.

Alitoroka kwasababu ulikuwa "wakati muafaka kufanya hilo".

Kumekuwa na wasiwasi mkubwa unaoongezeka Burundi juu ya mipango ya rais kuongeza muhula wa tatu kuongoza nchini humo.

Hatua hiyo inakiuka katiba na makubaliano ya Arusha ya mwaka 2000, yaliyomaliza mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yaliyodumu kwa miaka saba.

Inasemekana chama tawala cha CNDD-FDD kimegawanyika baina ya wale wanaomuunga mkono Bw Nkurunziza kuendelea kubaki madarakani, na wale wanaopinga.

Radjabu aliiambia BBC kuwa yeye bado ni mwenyekiti wa chama tawala na Rais Nkurunziza lazima alitambue hilo.

Friday 6 March 2015

MABAKI YA THOMAS SANKARA KUFUKULIWA

Thomas Sankara in 1986

Serikali ya Burkina Faso imeamuru kufukuliwa kwa mabaki ya Thomas Sankara, aliyekuwa rais wa nchi hiyo aliyeuawa katika tukio la kupinduliwa mwaka 1987.

Hatua hiyo inamaanisha mabaki hayo yanaweza kutambuliwa rasmi – ombi lililokuwa likisubiriwa kwa muda mrefu na wafuasi wa Sankara, waliotaka ushahidi kuwa mabaki hayo yalikuwa yake.

Bw Sankara – anayeonekana kama Che Guevara wa Afrika – alizikwa haraka katika mapinduzi yaliyoongozwa na mrithi wake, Blaise Compaore.

Bw Compaore aliachia urais baada ya maandamano makubwa kufanyika Oktoba mwaka jana, 2014.

Alipokuwa madarakani, mahakama ya Burkina Faso ilizuia ombi la familia ya Bw Sankara kutaka mabaki ya mwili wake kufukuliwa.

Bw Compaore amekuwa akikana kuhusika katika mauaji ya Sankara, akisisitiza “mambo yote yako wazi” na hana “la kuficha”.

Chanzo: BBC                         
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

Thursday 5 March 2015

WALIOKUWA WASHIRIKA WA BW MUGABE WAMSHITAKI



Zimbabwean President Robert Mugabe attending his inauguration and swearing-in ceremony at the 60,000-seater sports stadium in Harare 22 August 2013

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ameshtakiwa kwa kuwafurumusha kimakosa waliokuwa maafisa wawili waandamizi wa chama tawala.

Wawili hao walifukuzwa kwenye chama Desemba na Februari kwa madai ya kuunga mkono jaribio la kumpindua.

Ruagare Gumbo na Didymus Mutasa wamefungua kesi Mahakama Kuu ya Zimbabwe wakitaka amri itolewe ya wao kurejeshwa Zanu-PF.

Bw Gumbo aliiambia BBC kuwa Rais Mugabe ni “dikteta” na anatakiwa kuachia madaraka.

Wanataka pia mahakama ifute mabadiliko ambayo Rais Mugabe aliwasilisha kwenye mkutano wa chama Desemba iliyopita.

Wakifanikiwa, waliokuwa watu wake wa karibu sana rais huyo wataweza kuitisha mkutano wa kipekee wa chama ambapo kiongozi mpya anaweza kuchaguliwa kumrithi Bw Mugabe mwenye umri wa miaka 91.

Friday 27 February 2015

MWIMBAJI MAARUFU RWANDA AFUNGWA MIAKA 10


 Rwandan musician Kizito Mihigo in April 2014

Mwimbaji maarufu wa Rwanda amepewa kifungo cha miaka 10 gerezani baada ya kukutwa na hatia ya kuwa na mpango wa kumwuua Rais Kagame na kuchochea chuki dhidi ya serikali.

Awali Kizito Mihigo alikiri kosa na kuomba msamaha, ikimaanisha hukumu yake imepunguzwa.

Mwenzake aliyetuhumiwa naye, Cassien Ntamuhanga, mkurugenzi wa kituo cha redio cha Kikristo, amefungwa kwa miaka 25 jela kwa kosa la ugaidi na uchochezi.

Aliendelea kukana tuhuma zote.

Mihigo alikiri kuwasiliana kwa ujumbe mfupi wa simu na kundi la upinzani lenye makao makuu Afrika Kusini, la Rwanda National Congress (RNC).

Alifutiwa makosa ya ugaidi huku Ntamuhanga akifutiwa kosa la jaribio la kumwuua Rais Kagame.

Licha ya Mihigo kukiri makosa yote yanayomkabili, wakili wake baadae alisema kulikuwa hakuna ushahidi wowote wa kumtia hatiani.

Patrick Karegeya ni mmoja wa waanzilishi wa RNC, aliyekuwa mkuu wa ujasusi wa Rwanda ambaye aliwahi kuwa mshirika wa Rais Kagame.

Karegeya alikutwa amekufa nchini Afrika kusini mwaka jana huku washirika wake, familia na mamlaka za Afrika kusini zikiilaumu serikali ya Rwanda, iliyokataa kuhusika na mauaji hayo.

Sunday 22 February 2015

MBUNGE CANADA ALAUMU KUBANWA NA 'CHUPI'




Mbunge wa Canada alitoa kisingizio cha ajabu kuwahi kutolewa kwa kuondoka bungeni haraka – nguo ya ndani kumbana.

Ilivyoonekana nguo za ndani zilizombana zilimpa ugumu kukaa wakati walipokuwa wakipiga kura, mbunge wa upinzani Pat Martin alimwambia Spika aliyekuwa kamahanika.

Hatahivyo, aliwahi kurudi kupiga kura yake.

Bw Martin alizua vifijo na vicheko bungeni humo baada ya kuelezea sababu za kutoka kwa muda.

"Walikuwa wakiuza chupi za kiume kwa nusu bei na mie nikanunua kadhaa ambazo bila shaka zimekuwa ndogo kwangu. Napata ugumu kukaa kwa hakika.”

Spika wa bunge hilo alisema awali alimwamuru Bw Martin kukaa chini alipotaka kuondoka.

"Sikuelewa ufafanuzi wake wakati huo na sidhani kama naielewa sasa”, alisema.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

Tuesday 17 February 2015

OBASANJO WA NIGERIA ANG'ATUKA CHAMANI



Former Nigerian president Olusegun Obasanjo

Aliyekuwa rais wa Nigeria Olusegun Obasanjo ameng’atuka kutoka chama tawala cha People's Democratic Party (PDP) kabla ya uchaguzi wa Machi 28, akirarua kadi yake ya chama hadharani.

Bw Obasanjo alikuwa mkosoaji mkali wa Rais Goodluck Jonathan, anayetaka kugombea tena kwenye uchaguzi kupitia chama cha PDP.

Bw Jonathan anakabiliwa na changamoto kubwa kutoka mgombea wa upinzani Muhammadu Buhari.

Uchaguzi huo, uliotakiwa kufanyika Februari 14, uliahirishwa kutokana na sababu za kiusalama.

Mchambuzi wa BBC Nigeria alisema uamuzi wa Bw Obasanjo ni pigo kubwa kwa chama cha PDP, ikionyesha mgawanyiko ulioukikumba chama hicho huku ikipambana kuongeza muda wake wa uongozi wa miaka 15.