Tuesday 4 November 2014

SERIKALI YAKATA RUFAA KESI YA PISTORIUS



Oscar Pistorius pictured on 17 October 2014

Waendesha mashtaka wa serikali nchini Afrika Kusini wamekata rufaa dhidi ya mashtaka na hukumu aliopewa mwanariadha Oscar Pistorius.

Katika nyaraka za rufaa hiyo, waendesha mashtaka wamesema hukumu hiyo inawashangaza kutokana na kuwa nyepesi, isiyofaa na isingeweza kutolewa na mahakama yoyote makini.

Mwezi uliopita, Pistorius alianza kutumikia kifungo cha miaka mitano kwa mauaji ya kukusudia au kutokukusudia (culpable homicide) ya mpenzi wake, Reeva Steenkamp.

Alifutiwa mashtaka ya mauaji ya mpenzi wake huyo.

Pistorius anaruhusiwa kuomba kutumikia kifungo cha nyumbani kwa muda utakaobaki baada ya kukaa gerezani kwa miezi kumi.

Chanzo: AP, AFP


MGONGANO WA KISIASA ZAMBIA



Egar Lungu
Edgar Lungu ni kiungo muhimu kwenye chama cha Patriotic Front

Waziri wa ulinzi wa Zambia ambaye ana ndoto za kuwania urais, Edgar Lungu amerejeshwa kwenye nafasi yake ya ukatibu mkuu wa chama tawala, baada ya kufukuzwa siku ya Jumatatu na rais wa mpito Guy Scott.

Waandishi wanasema kumekuwa na mvutano wa madaraka unaochipuka wa nani atakayemrithi aliyekuwa rais Michael Sata, aliyeaga dunia wiki iliyopita.

Katika taarifa, iliyotiwa saini na wote wawili Bw Scott na Bw Lungu, chama tawala, the Patriotic Front, kilisistiza umuhimu wa umoja huku Zambia ikiomboleza kifo cha kiongozi huyo.

Usiku wa Jumatatu, polisi walirusha mabomu ya machozi kusambaza wafuasi wa Bw Lungu waliokasirishwa na kufurumushwa kwake.

Monday 3 November 2014

UWANJA WA NDEGE WA DAR 'WASHIKA MKIA'

 

Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Moses Malaki amesema uwanja wake umechakaa kiasi cha kukosa sifa za kuwa uwanja wa kisasa barani Afrika na dunia.

Kauli ya Malaki imekuja baada ya ripoti ya matokeo ya utafiti wa mtandao wa Sleeping in Airport uliyofanywa 2014 kuonyesha kuwa JNIA inashika nafasi ya nne kwa viwanja duni Afrika.

“Huo ni ukweli usiopingika kwa sababu uwanja ulijengwa zamani na miundombinu yake haikidhi mahitaji ya sasa…. hali ni mbaya,” alisema Malaki.

“Kiwanja kinakabiliwa na tatizo la miundombinu chakavu, vyoo visivyotosheleza na wakati huohuo kuzidiwa na wingi wa abiria, jambo linalosababisha huduma zake kuwa chini ya kiwango.

“Hatuwezi kuwa bora kwa uwanja huu… hebu fikiria uwanja uliojengwa kuhudumia watu milioni 1.2 kwa mwaka, sasa unahudumia watu 2.5 milioni, hapa lazima huduma zitakuwa chini ya kiwango na msongamo utakuwa mkubwa.”

Alisema katika kukabiliana na changamoto ya msongamano, ofisi yake iko katika hatua za kuongeza vizimba vya kugongea hati za kusafiria kutoka saba vya sasa na kuwa 21.

Alisema tayari wameshazungumza na Waziri wa Mambo ya Ndani kwa ajili ya kuongeza wafanyakazi, pia kuunganisha na kuwa sehemu moja kwa mlango wa abiria wanaowasili na wa ndani, kazi itakayokamilika wiki mbili zijazo.

MJUMBE WA MALAWI 'AMPUUZA' BW MUGABE



Thoko Banda
Thoko Banda amesema hatopuuza wajibu wake wa kutetea haki za bindamu kwasababu ya kazi

Mwanadiplomasia wa Malawi amekataa kazi ya kuwa balozi nchini Zimbabwe kwasababu anapinga udikteta, ameiambia BBC.

"Watu wenye hisia wanatakiwa kuwaunga mkono watu wa Zimbabwe, hasa wale wanaoishi katika hali ya umaskini," alisema Thoko Banda.

Mwaka 2006, iliripotiwa kuwa alimwita Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe "mjinga".

Bw Banda aliiambia BBC hatotumia maneno hayo tena.

Bw Mugabe amekuwa madarakani Zimbabwe tangu mwaka 1980 lakini amekana kukikuka haki za binadamu.

Serikali zote mbili hazijasema lolote kuhusu kauli hiyo ya Bw Banda.

Bw Mugabe anabaki kuwa kiongozi mwenye ushawishi mkubwa barani Afrika na anaungwa mkono na viongozi wengi wa bara hilo, licha ya kukosolewa sana na nchi za kimagharibi.


UNAPOJIFUNGIA NJE UKIWA 'UTUPU'

 

Vimbwanga vya WhatsApp

Habari nyingine:

Polisi wa Kenya 'wauawa Turkana' http://bit.ly/1o8IKHZ

Ukibakia shule wazawadiwa ng'ombe http://bit.ly/1wr71uy

Mauaji ya kutisha DRC http://bit.ly/1zrplWM

Shairi: Huna mvuto http://bit.ly/1DPWQQA

Sunday 2 November 2014

RISASI ZARINDIMA BURKINA FASO



People gather at the podium of the state TV headquarters in Ouagadougou, Burkina Faso, 2 November 2014
Waandamanaji wakiwa kituo cha televisheni cha taifa wakitarajia upinzani kutangaza lolote

Televisheni ya taifa ya Burkina Faso imetolewa hewani, muda mchache baada ya askari kufyatua risasi kwenye makao yake makuu, na kuwalazimisha waandamanaji na waandishi wa habari kutawanyika.

Wakati huo huo kwenye mji mkuu, Ouagadougou askari waliwatawanya maelfu ya waandamanaji na kuweka vizuizi eneo hilo.

Askari walishika madaraka siku ya Ijumaa baada ya kiongozi wa muda mrefu Blaise Compaore kuachia ngazi kufuatia maandamano ya siku kadhaa.

Umoja wa Mataifa umelaani jeshi kuchukua hatamu na kutishia kuweka vikwazo.

Mjumbe wa Afrika magharibi Mohamed Ibn Chambas alisema jeshi lazima liruhusu uongozi wa kiraia.

Jeshi lilimtangaza Lt Kanali Isaac Zida kuwa kiongozi wa serikali ya mpito siku ya Jumamosi.

Maelfu ya waandamanaji walikusanyika maeneo mbalimbali mjini Ouagadougou siku ya Jumapili kulipinga jeshi.

Opposition leader Saran Sereme adjusts her headscarf as she visits the national television headquarters in Ouagadougou on November 2
Kiongozi wa upinzani Saran Sereme alipofika kituo cha televisheni cha taifa kabla tu risasi kufyatuliwa

Kulikuwa na tafrani wakati kiongozi wa upinzani Saran Sereme na aliyekuwa waziri wa ulinzi Kwame Lougue walipowasili kwenye makao makuu ya televisheni hiyo ya taifa.

Watu hao waliokusanyika waliamini Be Sereme alikuwa anatarajia kutangaza kuongoza serikali hiyo ya mpito, mwandishi wa BBC aliyopo Ouagadougou Laeila Adjovi aliripoti.

Taarifa zinasema Jenerali mstaafu Lougue naye alikusudia kutangaza kutaka kuongoza nchi hiyo wakati huo pia.

Hata hivyo, muda mfupi baada ya kuwasili, risasi zikaanza kurushwa hivyo wafanyakazi na waandamanaji wakaanza kukimbia.


Saturday 1 November 2014

POLISI WA KENYA 'WAUAWA TURKANA'



 Turkana county, Kenya

Takriban maafisa saba wa polisi wameuawa na 17 hawajulikani walipo baada ya kutokea shambulio nchini Kenya, ripoti zinasema.

Maafisa hao walivamiwa ghafla na watu wa kabila moja katika kaunti ya Turkana wakati wa shughuli za ulinzi siku ya Ijumaa.

Maafisa ambao hawajulikani walipo ni polisi wa akiba. Gazeti la Standard limesema helikopta ya jeshi imepelekwa kuwasaka.

Turkana, uliopo kaskazini mwa nchi hiyo, ni kaunti maskini kuliko zote Kenya na ni ya pili kwa ukubwa nchini humo.

Vyanzo ndani ya jeshi la polisi vimeiambia redio ya Kenya, Capital FM kuwa “bado hali ni tete” na jenerali inspekta wa polisi ameambiwa asizuru eneo hilo.

Wiki iliyopita magazeti ya Kenya yaliripoti kuwa watu watano, wakiwemo maafisa polisi, waliuawa karibu na eneo la tukio hili la Ijumaa lilipotokea.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu

MAPENZI YA MTANDAONI, NOMAAAAA


   

Vimbwanga vya WhatsApp