Sunday 28 December 2014

RUSHWA, NGONO TATIZO MISS TANZANIA

Mkurugenzi wa Lino Agency International, Hashim Lundenga

Serikali imesema imeyafungia mashindano ya Miss Tanzania baada ya waandaaji kukiuka taratibu na kanuni huku pia yakitajwa kukithiri kwa rushwa ya ngono na upendeleo.

Mashindano hayo yalifunguliwa mwaka 1994, yamefungiwa kwa miaka miwili baada ya kuwapo kwa malalamiko kutoka kwa wananchi na washiriki.

Kaimu Katibu Mtendaji wa Bazara la Sanaa Tanzania (Basata), Godfrey Mngereza alisema jana kuwa Kamati ya Miss Tanzania kupitia kampuni yake ya Lino Agency, imekiuka kanuni na taratibu zinazoongoza mashindano hayo.

“Ni kweli kwamba tumeifungia Miss Tanzania kwa miaka miwili, lakini haya si maazimio ya tathmini iliyofanyika mapema mwezi huu, bali kulikuwa na vikao mbalimbali vilivyofanyika na si kimoja, ni uamuzi mgumu ambao umekuja kutokana na sababu maalumu,” alisema Mngereza.

GEORGE WEAH ASHINDA USENETA LIBERIA



 George Weah speaking at a campaign rally in Liberia

Aliyekuwa nyota wa soka George Weah ameshinda kwa kishindo katika uchaguzi wa seneta nchini Liberia, kwenye uchaguzi uliovurugwa na mlipuko wa Ebola.

Bw Weah alipata 78% ya kura zote kwa kiti cha kaunti ya Montserrado, ukiwemo mji mkuu Monrovia.

Alimshinda Robert Sirleaf, mtoto wa kiume wa Rais Ellen Johnson Sirleaf, ambaye alipata takriban 11%.

Idadi ndogo ya watu waliojitokeza kupiga kura, ambao mwanzo ulipangwa kufanyika mwezi Oktoba, ulitokana na wasiwasi wa kuenea kwa Ebola.

Udhibiti mkali wa kiafya uliwekwa kuzuia usambazaji wa ugonjwa huo.

Wengine walioshinda katika uchaguzi huo wa seneta ni pamoja na Jewel Howard-Taylor, aliyekuwa mke wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo aliyopo gerezani kwa sasa Charles Taylor, na aliyekuwa kiongozi wa waasi Prince Johnson. Wote wawili wamebaki na nafasi zao.

Bw Weah alishinda duru ya kwanza ya uchaguzi wa rais wa mwaka 2005, na kushindwa duru ya pili ambapo nafasi hiyo alipata Bi Johnson-Sirleaf.

Ni Mwafrika pekee kutajwa kuwa mwanasoka bora wa mwaka wa Fifa, aliposhinda mwaka 1995.


Saturday 27 December 2014

USHABIKI WA SOKA SAMBAMBA NA FUMANIZI



   

Vimbwanga vya WhatsApp

Na habari nyingine:

MAHAKAMA YA KIGAIDI SAUDIA 'YAWASHTAKI MADEREVA WANAWAKE'



Friday 26 December 2014

KESI YA ALIYEKUWA MKE WA RAIS WA I COAST YAANZA



Former Ivory Coast President Laurent Gbagbo and his wife Simone attending a ceremony in Abidjan in 2011
Aliyekuwa Rais wa Ivory Coast Laurent Gbagbo na mkewe walikamatwa mwaka 2001

Kesi ya aliyekuwa mke wa rais wa Ivory Coast, Simone Gbagbo, kwa madai ya kuhusika katika ghasia za baada ya uchaguzi miaka mitano iliyopita imeanza.

Mke wa aliyekuwa Rais Laurent Gbagbo ameshtakiwa pamoja na wafuasi wengine 82 wa mume wake.

Bw Gbagbo anasubiri kesi yake ianze kusikilizwa katika Mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita, ICC, kwa mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu.

Takriban watu 3,000 walikufa kutokana na ghasia, baada ya aliyekuwa rais kukataa kukubali kushindwa wakati wa marudio ya upigaji kura.

Bi Gbagbo, aliyewekwa kifungo cha nyumbani kwa miaka mitatu, ameshtakiwa kwa “jaribio la kuyumbisha usalama wa taifa”.

Aliyekuwa waziri mkuu Gilbert Ake N'Gbo na mkuu wa chama cha Ivorian Popular Front (FPI) Affi N'Guessan wanashtakiwa pia pamoja na Bi Gbagbo.  

Mume wake, aliyekuwa Rais Laurent Gbagbo, anakabiliwa na mashtaka manne ICC mjini  Hague, ikiwa ni pamoja na mauaji, ubakaji na udhalilishaji.

Bw Gbagbo, mwenye umri wa miaka 69, anayesisitiza kuwa hana makosa, ni wa kwanza aliyekuwa rais kufikishwa mahakama ya ICC.


MADEREVA WA KIKE SAUDIA WASHTAKIWA 'KIGAIDI'



 Loujain al-Hathloul at wheel of her car

Wanawake wawili kutoka Saudi Arabia waliotiwa kizuizini kwa kukiuka amri ya kupigwa marufuku kwa madereva wanawake, sasa kesi yao itasikilizwa kwenye mahakama ya ugaidi, wanaharakati walisema.

Loujain al-Hathloul, mwenye umri wa miaka 25, na Maysa al-Amoudi, 33, wamekuwa kizuizini kwa takriban mwezi mzima.

Kesi za wanawake hao zinaripotiwa kuhamishwa kutokana na maneno waliyoandika kwenye mitandao ya kijamii – badala ya kuendesha kwao magari, kulingana na wanaharakati.

Saudi Arabia ni nchi pekee duniani kukataza wanawake kuendesha gari duniani.

Wanaume pekee ndio hupewa leseni ya udereva – na wanawake wanaoendesha gari hadharani huwa hatarini kutozwa faini na kukamatwa na polisi.

Wanawake wa Arabuni wamefanya kampeni nyingi – zikiwemo kwenye mitandao ya kijamii – kutaka vizuizi vipunguzwe.

Thursday 25 December 2014

MSIKITI WACHOMWA MOTO SWEDEN



Firemen outside the mosque in Eskilstuna, Sweden, that was set alight - 25 December 2014

Mtu mmoja amechoma moto msikiti katika mji wa Eskilstuna nchini Sweden siku ya Alhamis, na kujeruhi watano, polisi walisema.

Takriban watu 15 hadi 20 walikuwa wakihudhuria swala ya mchana kwenye msikiti huo, ulio ghorofa ya chini, moto huo ulipozuka siku ya Krismasi.

Vyombo vya habari nchini humo vimeonyesha moshi na mvuke ukitoka dirishani kabla ya wazima moto kuutuliza moto huo.

Tukio hilo linatokea huku kukiwa na majadiliano makali Sweden juu ya sera za uhamiaji.

Wafuasi wa mrengo wa kulia wanataka kupunguza watu wanaotaka hifadhi nchini humo kwa 90%, huku vyama vengine vikitaka kudumisha sera za nchi hiyo za kiliberali.

 Msemaji wa polisi Lars Franzell alisema watu watano walipelekwa hospitali kupata matibabu baada ya kujeruhiwa kutokana na kuvuta pumzi wa moshi.

Mpaka sasa hamna aliyekamatwa kutokana na tukio hilo, Bw Franzell alisema.




BINTI ADAI WAZAZI WALIMKABIDHI KWA BOKO HARAM



Nigerian police present 13-year-old girl to reporters in Kano. 24 Dec 2014

Mtoto wa kike kutoka Nigeria mwenye umri wa miaka 13 ameelezea namna wazazi wake walipomkabidhi kwa wapiganaji wa Boko Haram ili ajitolee mhanga.

Binti huyo, akizungumza na waandishi wa habari iliyoandaliwa na polisi, alisema alipelekwa mjini Kano ambapo mabinti wengine wawili walilipua mabomu yao.

Takriban watu wanne walikufa katika shambulio la Desemba 10. Binti huyo alikamatwa, bado akiwa amevaa mabomu, polisi walisema.

Takriban watu 2,000 walikufa kutokana na mashambulio waliohusishwa nao wapiganaji hao mwaka huu.

Binti huyo aliwaambia waandishi wa habari kuwa wazazi wake walimpeleka kwa wapiganaji hao waliojificha msituni karibu na mji wa Gidan Zana katika jimbo ka Kano kaskazini mwa nchi hiyo.

Alisema mmoja wa viongozi wa kundi hilo alimwuuliza kama anajua maana ya kujitolea mhanga kutumia bomu.

"Walisema, 'Utaenda peponi ukifanya hivyo.' Nikasema 'Hapana siwezi.' Wakasema watanipiga risasi au kunirusha kwenye gereza."

Binti huyo hatimaye alisema  alikubali kushiriki kwenye shambulio hilo lakini "hakuwahi kuwa na nia ya kufanya hivyo".

Alisema alijeruhiwa baada ya mmoja wa mabinti hao kujilipua na kuishia hospitali ambapo mabomu hayo yaligunduliwa.

Haikuwa rahisi kuthibitisha taarifa ya binti huyo. Waandishi walisema hapakuwa na wakili wowote wakati wa mkutano hao wa waandishi wa habari.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu