Friday 28 November 2014

UCHAGUZI WA KWANZA KWA ELEKTRONIKI AFRIKA


 Screengrab of video introducing electronic voting machines to be used in Namibian elections

Raia wa Namibia leo wanachagua rais na wabunge – kwa kile kinachojulikana kuwa ni nchi ya kwanza kupiga kura kwa njia ya elektroniki barani Afrika.

Chama tawala cha South West Africa People's Organisation (Swapo) kinatarajiwa kushinda uchaguzi huo na waziri mkuu Hage Geingob kuwa rais.

Vyama vya upinzani vimekosoa mashine hizo za elektroniki zilizotengenezwa India, na kuonyesha wasiwasi kuwa upungufu wa karatasi unaweza kuchochea wizi wa kura.

Lakini kesi hiyo ilitupiliwa mbali na mahakama kuu wiki hii.

Takriban wapiga kura milioni 1.2 wana uwezo wa kupiga kura katika takriban vituo 4,000 vya kupiga kura nchini humo.

Maafisa kwenye vituo vya  upigaji kura watathibitisha kadi ya upigaji kura katika kifaa cha taifa kilicho na taarifa za wapiga kura.

Katika chumba cha kupigia kura, mpigaji kura huchagua chama anachotaka kwa kubonyeza kitufye kwenye chombo maalum cha elektroniki.

Maafisa wa uchaguzi wanaamini matokeo yatatolewa saa 24 baada ya upigaji kura kumalizika.
Vyama 16 vinagombea nafasi za ubunge na wagombea wa urais ni tisa.


Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu
 

MWANAMUME KUJITITIMUA, KISHA? HA HA HA

Thursday 27 November 2014

MABINTI WAWILI WA INDIA 'WALIJINYONGA'



Villagers collect near tree where the girls were found in Badaun
Wanavijiji wenye hasira waliandamana kwenye mti ambapo mabinti hao walikutwa wamenyongwa wilaya ya Badaun
Mabinti wawili wa India waliokutwa wakining’inia kwenye mti mwezi Mei inasemwa kuwa walijiua na hawakubakwa na watu wengi kisha kuuliwa, wachunguzi wa serikali walisema.

Uamuzi huo umetolewa baada ya uchunguzi wa miezi kadhaa uliofanywa kufuatia shinikizo kutoka sehemu mbalimbali duniani.

Wanaume watatu waliokamatwa kuhusishwa na tukio hilo katika jimbo la Uttar Pradesh kaskazini mwa nchi hiyo waliachiwa kwa dhamana mwezi Septemba.

Haiko wazi kwanini mabinti hao walijiua. Waandishi wanasema kuna maswali mengi yasiyo na majibu.

Wanaharakati wa masuala ya wanawake wanasema hawajaridhika na matokeo hayo na kutaka chombo hicho cha CBI kiendelee na uchunguzi.

Ndugu hao wawili, wanaodhaniwa kuwa na umri wa miaka 14 na 15, walikutwa wamejinyonga kwenye mwembe Mei 28.

Hali ya kuwepo maelezo machache ya sababu za mabinti hao kujiua kumesababisha wengi kuhoji matokeo hayo ya CBI.

PELE ALAZWA BRAZIL



 

Nyota wa soka wa Brazil Pele amehamishiwa katika idara maalum kufuatia kupata maambukizi kwenye njia ya haja ndogo.

Hospitali ya Albert Einstein mjini Sao Paulo imesema nyota huyo mwenye umri wa miaka 74 aliyeshinda mara tatu kwenye kombe la Dunia amehamishwa baada ya “kuumwa mara kwa mara”.

Ripoti zilisema Pele, aliyelazwa siku ya Jumatatu, alikuwa katika chumba maalum cha wagonjwa mahututi.

Pele, mshindi katika Kombe la Dunia mwaka 1958, 1962 na 1970, awali alitolewa hospitalini Novemba 13 baada ya kufanyiwa upasuaji na kutolewa mawe kwenye figo.

Inaeleweka kwamba wakati huduma maalum ni zaidi ya huduma ya kawaida, lakini si hatari sana kama ilivyo kwenye chumba maalum cha wagonjwa mahututi, na Mbrazil huyo ambaye bado anaheshimika kama mchezaji wa kipekee kuwepo duniani – bado anaweza kutembelewa na wageni.


GHANA YAKUMBWA NA KASHFA YA 'DAWA ZA KULEVYA'


map





Upande wa upinzani nchini Ghana umetoa wito wa kuwepo  uchunguzi wa bunge katika madai kuwa muuzaji mmoja wa dawa za kulevya aina ya cocaine alikuwa na uwezo wa kuingia katika sehemu maalum ya mapumziko ya rais kwenye uwanja mkuu wa ndege nchini humo.

Anayedaiwa kuwa muuzaji alikamatwa nchini Uingereza, huku maafisa watatu wamefunguliwa mashtaka Ghana.

Tukio hilo limekuwa gumzo miongoni mwa raia wa Ghana, wakati upinzani na chama tawala wakishutumiana kuhusu biashara ya dawa za kulevya.

Afrika magharibi ni njia kuu ya mpito ya kupitisha dawa hizo kimagendo barani Ulaya.

Serikali imekana kuhusika kwa namna yoyote na tukio hilo kwa kile redio za nchi hiyo zilivyoiita “kashfa ya cocaine”.

Rais John Mahama pia amekana vikali taarifa kuwa Bi Nayele Ametefe aliyekamatwa uwanja wa ndege wa Heathrow Novemba 9, ana uhusiano na familia yake.




Wednesday 26 November 2014

RIPOTI YA TEGETA ESCROW ILIYOSOMWA BUNGENI, TZ

Yasemekana hawakulala Wabunge hawa, walikesha hivi wakiilinda ripoti
                                            


 Ripoti hii ya kusikiliza kwa bahati mbaya imeanzia katikati japo ni dakika chache tu za mwanzo


Chanzo: wavuti.com

ZITTO AHOJIWA NA BBC KUHUSU KASHFA YA ESCROW


 
Kashfa ya TegetaEscrow inazidi kufukuta nchini Tanzania. Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA) pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) leo aliwasilisha ripoti ya uchunguzi katika bunge la nchi hiyo. Katika matangazo ya Dira ya Dunia TV, Zuhura Yunus alimhoji mbunge huyo kujua zaidi.

Tuesday 25 November 2014

MAHAKAMANI KWA KUMFANYA BINTI KUWA 'MWEUPE'





 






















Halle Berry amempeleka aliyekuwa mpenzi wake Gabriel Aubry mahakamani kwa madai ya kutaka kubadilisha muonekano wa binti yao ili awe mweupe.

Anadai Aubry amezinyoosha nywele za Nahla zilizojinyonganyonga na kuzipaka rangi kwa nia ya kumfanya asionekane Mmarekani mweusi.

Nyaraka za mahakamani zinamshutumu Aubry kwa kumsababishia “uharibifu wa kisaikolojia na wa mwili” kwa binti yao mwenye umri wa miaka sita na kumsababishia aanze kuwaza “kwanini muonekano wake wa asili hautoshi ”.

 “Nataka mimi na Gabriel tuchukue uamuzi pamoja juu ya binti yetu, ukuaji wake, maendeleo yake na maisha yake kwa ujumla,” alisema Berry kwenye nyaraka hizo.

Wakili wa Berry, Steve Kolodny, ndie aliyekuwepo mahakamani siku ya Jumatatu pamoja na Aubry.
Jaji alitoa uamuzi kuwa hakuna mzazi hata mmoja anayeweza kubadili muonekano wa Nahla kutoka asili yake.

Wapenzi hao waliachana mwaka 2010 baada ya kuwa pamoja kwa miaka minne.


Chanzo: www.independent.co.uk
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu
 

WAKENYA WAKIMBIA BAADA YA SHAMBULIO


Protesters in Nairobi (25 November 2014)

Mamia ya watu wamekimbilia uwanja mdogo wa jeshi katika mji wa Mandera nchini Kenya kukiwa na hofu ya wapiganaji kuanzisha mashambulio upya.

Wengi waliokimbia nia wafanyakazi wa serikali wasio Waislamu wanaotaka serikali iwaondoshe eneo hilo, mwandishi wa habari wa BBC alisema.

Kundi la al-Shabab linalohusishwa na Al-Qaeda liliua watu 28 kwenye shambulio la basi siku ya Jumamosi.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta anapata shinikizo kubwa kusimamisha mashambulio hayo.

Makao makuu ya Al-Shabab yako nchi jirani ya Somalia, lakini limeanzisha mashambulio Kenya tangu mwaka 2011, baada ya Kenya kupeleka majeshi mpakani kusaidia kupambana na wapiganaji.

Mwandishi wa BBC aliyopo kwenye mji mkuu, Nairobi, alisema upinzani na baadhi ya wabunge wa chama tawala wametoa wito wa idara ya usalama kubadilishwa kabisa, ikiwemo kufukuzwa kwa waziri wa mambo ya ndani Joseph Ole Lenku na mkuu wa polisi David Kimaiyo.