Tuesday, 10 February 2015

MBUNGE AUAWA NA AL-SHABAB SOMALIA



File photo of al-Shabab fighters, February 2011

Mbunge mmoja wa Somalia amepigwa risasi na kufa mjini Mogadishu na wapiganaji wa al-Shabab, maafisa walisema.

Abdullahi Qayad Barre aliuawa karibu na kasri ya rais baada wa watu wenye silaha kumfyatulia risasi kwenye gari lake.

Msemaji wa al-Shabab alisema kundi hilo limehusika na shambulio hilo, na litalenga wabunge wengine.

Kifo cha Barre kimetokea huku kukiwa na ulinzi mkali wakati wabunge walipokusanyika kupiga kura ya kuidhinisha baraza jipya la mawaziri au la.

Ni mfululizo wa mauaji dhidi ya wanasiasa nchini humo.

Takriban wabunge watano waliuawa mwaka jana, lakini Barre ni wa kwanza kuuawa mwaka huu 2015.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na mwandishi wetu                                                                                   

Monday, 9 February 2015

BOB MARLEY 'UTOTONI'

     

Vimbwanga vya WhatsApp

MAMBO 5 YANAYOKWAMISHA BIASHARA



Wafanyabiashara wengi hukumbwa na changamoto nyingi katika uendeshaji wa shughuli zao za biashara. Changamoto hizi ndizo zinaweza pia kuwa utofauti wa biashara zinazokua na zile zinazokufa.

Makala hii inachambua mambo muhimu ambayo huwa ni mzigo mzito kwa wajasiriamali hata kufikia hatua ya kuathiri biashara zao, na pia makala hii inaonyesha baadhi ya njia za kukabiliana na changamoto hizo.

1. Mtaji

Kikwazo hiki hujitokeza katika mitazamo mitatu, kwanza wakati wa kutaka kuanzisha biashara, pili wakati biashara imeshaanza ila fedha hazitoshi kuendesha vema, na tatu pale mfanyabiashara anapokusudia kupanua biashara yake. Ili kukabiliana na kikwazo cha mtaji yafuatayo yanaweza kusaidia:-

Kuanza biashara kidogo kidogo: Hii namaanisha kuwa kufikiria namna ambazo unaweza kuanzisha biashara kwa mtaji mdogo na wakati huo huo ukafanya kwa ufanisi. Hii inaweza kwa kuchunguza kwa umakini gharama zisizo za lazima, mambo ambayo unaweza fanya wewe mwenyewe au kusaidia na watu wengine bila kuajiri, pia chunguza aina ya bidhaa ambazo kweli ni za lazima kuanza nazo. Kutunza taarifa za biashara yako kwa ufasaha na kuwa na muundo bora wa uongozi, hii itakusaidia kuwa kutimiza masharti ya benki, na wadau mbalimbali wa sekta ya fedha ambao wanaweza kukuongezea mtaji.

Zingatia pia kuwa na mali zisizohamishika, na pia kuna na mahusiano mazuri na wadau mbalimbali kwani wao wanaweza kuwa vyanzo vya kukupatia mtaji.

2. Muundo wa biashara

IVORY COAST YASHINDA KOMBE LA AFRIKA 2015

Ivory Coast wameshinda taji la Kombe la Afrika mwaka 2015
Ivory Coast wameshinda taji la Kombe la Afrika mwaka 2015 kwa mikwaju 9 ya penati Ghana 8

Timu ya soka ya Ivory Coast imenyakuwa taji la Kombe la Afrika la mwaka 2015 kwa kuitandika timu ya Ghana kwa mikwaju ya penati.

Ivory Coast imeshinda kwa mikwaju 9 ya penati huku Ghana ikipata mikwaju 8.

Boubacar Barry, 35, ndiye aliyeibuka kidedea kwa kufunga penati ya mwisho baada ya mlinda mlango wa Ghana Razak Braimah kukosa penati.

Ghana walipata penati 8 huku Ivory Coast wakishinda kwa penati 9
Ghana walipata penati nane huku Ivory Coast wakishinda kwa penati tisa

Mlinda mlango mkongwe wa Ivory Boubacar Barry ndiye nyota wa mchezo wa leo.

Mashindano hayo yalikuwa yanafanyika nchini Equatorial Guinea.


Chanzo: taarifa.co.tz

Sunday, 8 February 2015

MASHABIKI WA MPIRA WAZUA GHASIA, 14 WAFARIKI



 Egyptian firefighters extinguish fire from a vehicle outside a sports stadium in a Cairo"s northeast district

Takriban watu 14 wamefariki dunia katika mapambano yaliyozuka baina ya mashabiki wa mpira na polisi nje ya uwanja wa mpira mjini Cairo, chombo cha habari cha taifa cha Misri kimeripoti.

Mashabiki wa klabu ya mpira ya Zamalek walijaribu kuingia uwanjani kutazama mechi bila tiketi, na kuchochea ghasia hizo, maafisa walisema.

Vurugu hizo zilianza kabla ya mechi baina ya pande za Zamalek na ENPPI.

Februari 2012, zaidi ya watu 70 walikufa katika ghasia zilizozuka baada ya mechi huko Port Said.


DEREVA ALIYEFUKUZWA AKUSUDIA KUUA 50


 East Africa bus. (AP)



Polisi nchini Uganda walisema walimkamata dereva aliyejaribu kuligonga basi kwenye mto ulojaa mamba kwa nia ya kuua abiria 50 waliokuwa kwenye chombo hicho baada ya kufukuzwa kazi.

“Tulipojua kuhusu utekajinyara huo, tuliweka vizuizi  kabla ya  mto huo ..tulimvamia halafu tukamkamata.” Alisema Denis Namuwooza,  mkuu wa polisi katika wilaya ya Kasese kusini-magharibi mwa Uganda.

Dereva huyo, ambaye polisi walisema alifukuzwa kutokana na ulevi, iliripotiwa alikusudia kulirusha basi hilo huko Kazinga, mto ambao aghlabu hujaa viboko, ambao huunganisha maziwa mawili makubwa katika mbuga ya wanyama ya Queen Elizabeth nchini Uganda.

Aliwaambia abiria "atakufa pamoja na wao kwa kulirusha basi Kazinga, “ alisema mmoja aliyenusurika, Dinah Mwagale Mudusu, akizungumza na chombo cha habari cha Uganda.

Chanzo: AFP 
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu                                                    

UCHAGUZI WA MWEZI HUU NIGERIA WAAHIRISHWA



People hold signs to protest against the postponement of elections, in Abuja, Nigeria, 7 February 2015
Mapema Jumamosi, waandamanaji wengi wametoa wito wa uchaguzi kuendelea kama ilivyopangwa

Upinzani wa Nigeria umesema hatua ya kuahirisha uchaguzi wa rais wa Februari 14 kwa wiki sita “una athari kubwa kwa demokrasia”.

Tume ya uchaguzi imesema imesogeza tarehe ya upigaji kura kwasababu majeshi yaliyotakiwa kufanya ulinzi kwenye vituo vya kupigia kura yamesambazwa kupambana na Boko Haram

Kuahirishwa kwa uchaguzi huo kumeifurahisha chama tawala, lakini Marekani imesema “imesikitishwa”

Nigeria imekuwa ikipambana na wapiganaji wa Boko Haram kaskazini-mashariki mwa nchi hiyo.

Maelfu ya watu wamekufa kutokana na mapigano ya wapiganaji hao katika kipindi cha miaka sita iliyopita.

Boko Haram pia imeanza kushambulia majirani wa Nigeria: siku ya Jumapili, kwa mara ya pili katika siku tatu, wapiganaji hao wameshambulia mji wa Diffa mpakani mwa Niger.

Takriban mtu mmoja alifariki dunia kwenye mlipuko katika soko la mji huo, huku baadhi ya walioshuhudia wakisema mtu aliyejitoa mhanga ndiye kahusika.

BABA WA KIM KARDASHIAN APATA AJALI



Bruce Jenner

Polisi Los Angeles wamethibitisha nyota wa kipindi cha TV Bruce Jenner amehusika kwenye ajali iliyosababisha kifo cha mwanamke mmoja.

Jenner mwenyewe hakujeruhiwa, lakini wengine saba walipelekwa hospitalini.

Mwanamke mwenye umri wa miaka ya 70 alitangazwa kufariki dunia kwenye eneo la tukio huko Malibu.

Msemaji wa polisi wa LA alisema hapakuwa na dalili zozote kuwa Jenner, baba wa kambo wa Kim Kardashian, akifuatiliwa na mapaparazzi.

Msaidizi wa Jenner, Alan Nierob, alisema baba huyo mwenye umri wa miaka 65 hakuumia.

Sajeni Philip Brooks, kutoka iadara ya polisi ya Los Angeles, alisema gari aina ya Cadillac Escalade ya Bruce Jenner iliigonga kwa nyuma gari aina ya Lexus sedan, ambayo nayo ilikuwa imeigonga upande wa nyuma wa gari aina ya Toyota Prius.

Lexus hiyo ikaingia kwenye foleni iliyopo mstari mwengine na kugongana na gari jeusi aina ya Hummer.

Polisi walisema Jenner alishirikiana vyema na wachunguzi katika eneo la tukio na hakukutwa na pombe mwilini alipopimwa. Pia alipimwa damu.

Jenner alishinda dhahabu kwenye mashindano ya Olimpiki mwaka 1976 ya ‘decathlon’ lakini anajulikana zaidi kwenye kipindi maarufu cha TV Keeping Up With The Kardashians.


'KINYESI' CHA BINTIYE KUMWONGEZEA UZITO



Toilet paper

Mwanamke mmoja ameongezeka uzito kwa kiwango kikubwa baada ya kuhamishiwa bakteria kutoka kwenye kinyesi ‘stool transplant’ cha binti yake, madaktari walisema.

Ni utaratibu halali wa kitabibu kuhamishia bakteria wazuri kwenye utumbo ulioathirika, lakini madaktari wa Marekani wanahisi huenda imeathiri eneo la kiuno.

Ghafla aliongezeka kwa kilo 16 na sasahivi anachukuliwa kama mtu mwenye maradhi ya unene kupindukia.

Mtaalamu mmoja wa Uingereza alisema uhusiano baina ya bakteria wa tumboni na unene kupindukia bado hauko wazi.

Kuhamishiwa bacteria ‘wazuri’ wa kinyesi kwenye kiungo cha mtu mwengine hasa kwenye utumbo ‘faecal microbiota transplant’ – ambao baadhi huita "transpoosion" – kumeungwa mkono rasmi na huduma za kutoa afya za Uingereza mwaka jana.

Tiba mpya

Saturday, 7 February 2015

ALI KIBA AZUNGUMZIA BIFU LAKE NA DIAMOND



Hatimaye staa wa Bongofleva Ali Kiba amekiri kuwa yuko katika bifu na mwanamuziki mwenzie Diamond Platnumz kwa zaidi ya miaka mitatu sasa.

Kauli hiyo ya Ali Kiba inapingana na ile ya hivi karibuni iliyowahi kutolewa na Mwenyekiti wa Kamati za bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe alisisitiza kuwa wanamuziki hao hawana tofauti zozote na kwamba ni watu tu ndio wanakuza suala hilo.

Hata hivyo, juzi Ali Kiba aliliambia gazeti hili kuwa ni kweli kuna ugomvi baina yao, huku akisisitiza kwamba tofauti yao ilianza mwaka 2012. Wakati Ali Kiba akifunguka kuhusu bifu hilo hali imekuwa tofauti kwa Diamond ambapo amekaririwa mara kadhaa kuwa hana tofauti yeyote na mwanamuzi huyo ambaye wanatoka mkoa mmoja wa Kigoma na kuunganisha Kundi la Kigoma All Stars. Akizungumza wakati akijibu maswali mbalimbali katika mahojiano maalumu, mwanamuziki huyo pia alielezea mambo mengi kuhusu muziki wake na hii ni sehemu ya mahojiano hayo;

Swali: Nini chanzo cha bifu lako na Diamond?

Ali Kiba: Hakuna kiini kwa sababu nadhani hayo mimi aaah.…Kiukweli haya tuliyamalizaga muda mrefu …Labda watu wahisi kwamba kipindi kile alichonifuta katika wimbo wake (alisema bila kufafanua jina la wimbo) na yeye alivyosema kwamba nimemfuta katika wimbo wangu ‘Single Boy’, mimi sijawahi kurekodi na Diamond katika wimbo wangu hata mmoja na huo niliimba na Lady Jaydee.

Yeye ndiye aliyesema kwamba nilimfuta katika wimbo ule, ila ukweli ni kwamba hatukuwahi kuingia pamoja studio, nilimshauri tufanye wimbo mwingine lakini siyo ule kwa sababu nimeshaimba na Lady Jay Dee.

Swali: Umeshawahi kuwa karibu na Diamond?