Kifo ni 'biashara' kubwa
Ikiwa zaidi ya watu
nusu milioni hufariki dunia Uingereza kila mwaka, biashara ya mazishi
inatengeneza takriban dola bilioni mbili katika mapato ya kila mwaka,
kulingana na kampuni ya utafiti ya masoko Ibis World.
Takriban
makampuni 1,500 huajiri watu 20,105, na mapato yanatarajiwa kuongezeka
kwa 4.7% kufikia mwisho wa mwaka 2014, kutokana na ongezeko la ushindani
wa eneo la kuzika na ndivyo idadi ya watu wanaotaka kuchomwa
inaongezeka.
Kukiwa na soko kubwa na lenye faida kubwa, haishangazi kuona makampuni ya teknolojia yamekuwa yakitolea macho huduma za mazishi.
Usia wa Video
Usia
wako wa mwisho, kwa mfano ni programu tumishi ya iphone "app"
inayomruhusu yoyote kuweka ujumbe wa mwisho kwa wapendwa wao kwa njia ya
"usia wa video" ambao utaonekana wakishafariki dunia.
Unatengeneza
na kupakua video binafsi yenye usia na halafu unakuwa na neno lako la
siri QR code – Ni bar code inayosomeka kwenye simu za kisasa – ambayo
humpa mtu unayemwamini unayehisi atakuwa hai utakapofariki.
Ukishafariki
dunia, mtu huyo uliyemwamini atatia saini kwenye programu tumishi kwa
kutumia alama hiyo ya siri na atapata barua pepe itakayokuwa na ujumbe
wako wa mwisho. Baada ya hapo ujumbe huo utatumwa moja kwa moja kwa watu
wote uliowakusudia.
Kampuni hii inakiri kuwa "katika nchi nyingi,
usia kupitia video haiwezi kuwa mbadala wa usia wa maandishi”, lakini
kwa malipo ya ziada, Usia wako wa mwisho unatoa fursa kwa video yako
kutumika kisheria kwa kile kinachoitwa ”mchakato mwepesi”.
"Kifo
bila shaka ni jambo la huzuni lakini halikwepeki katika maisha ya
mwanadamu na ni rahisi zaidi kuacha ujumbe wa mwisho au usia kupitia
video kuliko njia iliyozoeleka, inayomhusisha mwanasheria na mashahidi,”
Wolfgang Gobler, mkurgenzi mkuu na muasisi wa Usia Wako, aliiambia BBC.
Anaamini teknolojia itaendelea kushawishi huduma za mazishi Uingereza na dunaini kote.
"Kutakuwa
na biashara nyingi zinazohusiana na mazishi siku za usoni.
Nimeshakutana na wengine ambao ndio kwanza wanaanza huduma hizo za
maisha na vifo," amesema.
Chanzo: BBC.
Imetafsiriwa na Mwandishi wetu