Thursday 8 January 2015

AL-SHABAB YAUA 'MASHUSHUSHU WA CIA NA ETHIOPIA'



Armed members of the militant group al-Shabab attend a rally on the outskirts of Mogadishu, Somalia in this February 2012 file photo.

Kundi la wapiganaji la Somalia al-Shabab limewaua kwa kuwamiminia risasi watu wanne wanaoshutumiwa kuwa ‘mashushushu’ wa shirika la Marekani CIA na mashirika mengine ya kijasusi.

Watu hao, wakiwemo wanajeshi wawili wa serikali, walipigwa risasi mbele ya mkusanyiko wa watu wengi katika mji wa Bardhere kusini mwa nchi hiyo, walioshuhudia walisema.

Mahakama inayoendeshwa na al-Shabab awali iliwatia hatiani kwa kufanya uchunguzi kwa niaba ya CIA, Ethiopia na serikali ya Somalia.

Mashambulio ya anga ya Marekani yameua makamanda wawili waandamizi wa al-Shabab katika miezi ya hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment