Monday 12 January 2015

MARUFUKU KUTENGENEZA 'SNOWMEN' SAUDI ARABIA


 

Huku sehemu chache za Saudi Arabia zikipata  theluji kwa nadra, fatwa iliyotolewa ya kupiga marufuku kutengeneza sanamu ya mtu kwa theluji ‘snowmen’ uliotolewa na kiongozi wa Kiislamu umekuwa ukisambaa kwa kasi.

Uamuzi huo uliotolewa na Sheikh Mohammed Saleh al-Munajjid ambaye ni maarufu sana unaonekana ulitolewa muda mrefu tu.

Sheikh huyo ametangaza kuwa kutengeneza sanamu huyo ni sawa na kutengeneza taswira ya binadamu, jambo ambalo linapigwa marufuku na dini ya Kiislamu.

Uamuzi wake huo umekosolewa na wengi kwenye mtandao wa kijami wa Twitter, huku raia kadhaa wa Saudia wameweka picha si tu za ‘snowmen’ lakini pia ngamia kwa kutumia theluji na ma biharusi kwa theluji.

Chanzo: Mtandao wa Sheikh

No comments:

Post a Comment