Sunday 18 January 2015

THAILAND KUITAMBUA JINSIA YA TATU?



 There's a perception that transgender people are well accepted in Thailand, due to the availability of gender reassignment surgery, as seen here in Bangkok. But challenges persist, says advocates.

Thailand, hivi karibuni inaweza kuanza kutambua jisnia ya tatu kwa mara ya kwanza kwenye katiba ya nchi hiyo.

"Ni haki ya binadamu kama ulizaliwa mwanamme au mwanamke na unataka kubadili jinsia yako au kuwa na maisha ya jinsia nyingine." Alisema Kamnoon Sittisamarn, msemaji wa kamati ya rasimu ya katiba, inayofanyia kazi rasimu mpya nchini humo.

"Watu wanatakiwa kuwa na uhuru wa kubadili jinsia na wanatakiwa kupata ulinzi sawa kutoka kwenye katiba na sheria na kupewa haki sawa."

Jinsia ya tatu inamaanisha kuwa mtu hatotakiwa kujitambulisha kama mwanamme au mwanamke, na kumpa haki ya kujitambulisha kivyake.

Iwapo itapitishwa , Thailand itajiunga na nchi kadhaa za bara la Asia, zikiwemo India, Pakistan na Nepal, ambazo hivi karibuni zimekubali kutambua jinsia ya tatu.


Chanzo: edition.cnn.com
 

 

No comments:

Post a Comment