Monday 19 January 2015

ASAMOAH GYAN KUCHEZA DHIDI YA SENEGAL?



 Asamoah Gyan

Kapteni wa Ghana Asamoah Gyan anaugua “malaria” na huenda asiweze kucheza dhidi ya Senegal siku ya Jumatatu.

Shirikisho la Mpira la Ghana lilisema mshambuliaji huyo alilazwa hospitalini huko Mongomo siku ya Jumamosi jioni na kutolewa Jumapili asubuhi.

Ugonjwa huo “uligunduliwa mapema” na Gyan anaendelea vizuri baada ya kupata matibabu.

Kiongozi wa timu ya Senegal Alain Giresse lazima aamue kuhusu afya ya Sadio Mane, ambaye amekuwa hachezi baada ya kujeruhiwa mguu.

Mchezaji huyo wa Southampton alijumuishwa kwenye timu hiyo licha ya klabu yake kusisitiza kuwa hatokuwa na afya nzuri ya kucheza.

Chanzo: BBC                                                

No comments:

Post a Comment