Monday 19 January 2015

BAKHSHISHI ATAKAYETOA TAARIFA YA ALBINO ALIYETOWEKA



A policeman holds up a picture of missing albino girl Pendo Emmanuelle Nundi

Polisi wa Tanzania wamesema watatoa tuzo kwa yeyote atakayetoa taarifa utakaoweza kusaidia mtoto wa kike albino ambaye hajulikani alipo anayehofiwa kutekwa kwa minajil ya  kupata viungo vyake vya mwili.

Pendo Emmanuelle Nundi, mwenye umri wa miaka 4, alitekwa mwezi uliopita. Baba wa binti huyo ni miongoni mwa watu 15 waliokamatwa kutokana na kutekwa huko.

Viungo vya mwili wa albino, husakwa na waganga wa kienyeji.

Tanzania imewapiga marufuku waganga wa kienyeji wanaopiga ramli katika jitihada za kuzuia mashambulio dhidi ya albino.

Polisi wameahidi kutoa shilingi milioni tatu za Kitanzania sawa na $1,700 kujaribu kumtafuta binti huyo ambaye hajulikani alipo “mfu au hai”.

Wajomba zake wawili binti huyo nao pia wamekamatwa kama sehemu ya uchunguzi.

                                                          

No comments:

Post a Comment