Friday 9 January 2015

MTOTO WA JACKIE CHAN AFUNGWA JELA





Jaycee Chan, mtoto wa kiume wa muigizaji nyota Jackie Chan, amefungwa jela miezi sita kwa kosa linalohusiana na dawa za kulevya.

Chan, mwenye umri wa miaka 32, alikiri kosa kwenye mahakama ya wilaya ya Dongcheng, Beijing kwa “kuhifadhi watu wengine kutumia dawa za kulevya.”

Polisi walivamia nyumbani kwake mwezi Agosti na kukuta zaidi ya gramu 100 za marijuana.

Alikabiliwa na kifungo cha miaka mitatu.

Kukamatwa kwake kulifanyika wakati wa msako mkali wa dawa za kulevya China ambapo watu maarufu kadhaa walijikuta wakikamatwa.

Juni 2014, Rais Xi Jinping walimwamuru polisi kutumia hatua kali kuzuia matumizi ya dawa za kulevya.

Kukiri kwa mtoto wa mmoja wa waigizaji maarufu China kunatoa ujumbe muhimu kutoka serikali ya China: hakuna mwenye kinga ya kukamatwa inapokuja suala la dawa za kulevya.

No comments:

Post a Comment