Monday 5 January 2015

KAMPUNI YA POMBE KUTUMIA PICHA YA GANDHI



 Gandhi Bot beer

Kampuni moja ya pombe ya Marekani imeomba radhi kwa kutumia picha ya shujaa wa uhuru wa India Mahatma Gandhi kwenye maokpo yake ya bia, taarifa zinasema.

Hatua hiyo ya kampuni ya New England imefanyika baada ya kesi kufunguliwa kwenye mahakama ya India ikisema hatua hiyo “imemdhalilisha” kiongozi huyo.

Gandhi aliongoza mapambano bila vurugu dhidi ya utawala wa Kiingereza nchini India.

Aliuawa Januari,1948, miezi kadhaa baada ya India kupata uhuru.

Pombe hiyo yenye picha ya kiongozi huyo inaitwa Gandhi-Bot.

Katika mtandao wake kampuni hiyo inasema bia hiyo ni “ni namna ya kujitakasa na kusaka ukweli na mapenzi".

Wakili mmoja amefungua kesi mjini Hyderabad, kusini mwa India, akidai kutumia picha ya Ghandi kwenye makopo ya pombe ni “la kulaaniwa” na la kuadhibiwa kutokana na sheria za India.

Kampuni hiyo ilisema inaomba radhi kwa yeyote waliyemwuudhi. Na hakuna dalili zozote za kampuni hiyo kuondosha picha hiyo.

Matt Westfall, mkuu wa kampuni hiyo alisema "wajukuu wa Ghandi wameiona picha hiyo na wameonyesha kuvutiwa nayo” Haikuwa wazi ni ndugu gani kampuni hiyo ilikuwa ikiwazungumzia hasa.

Alisema ana matumaini bidhaa hiyo itawavutia watu “kujifunza zaidi kuhusu Mahatma Gandhi na mbinu zake za kutotumia vurugu. Wahindi wengi hapa Marekani wameridhishwa na hatua hiyo.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment