Monday 5 January 2015

NEPAL YAANZISHA MABASI YA WANAWAKE TU

 Four women-only minibuses are currently operational

Huduma  ya basi ya wanawake pekee imeanzishwa kwenye mji mkuu wa Nepal, Kathmandu kupunguza kudhalilishwa kijinsia katika mji wenye njia zilizojaa watu wengi.

Mwenyekiti wa kampuni hiyo alisema nia ni kufanya wanawake wajisikie raha na salama.

Magari manne yenye viti 17 kila mmoja yatafanya safari zake kwenye barabara kuu muda wa shughuli nyingi.

Takriban robo ya mabinti wamedhalilishwa kijinsia katika usafiri wa umma, kulingana na utafiti wa Benki ya Dunia ya mwaka 2013.


Four 17-seat women-only minibuses will run on key routes in Kathmandu during rush hour
Lengo mwishowe ni wafanyakazi wote wa mabasi hayo wawe wanawake

Mabasi yote Kathmandu hutakiwa kuachia idadi kadhaa ya viti kwa „wanawake tu” kisheria, lakini wakosoaji wanasema sheria hiyo haitekelezwi.

Kwa sasa kuna kondakata mmoja tu mwanamke katika kampuni hiyo lakini Bw Bharat Nepal, mkuu wa jumuiya ya usafiri alisema nia mwisho ni wanawake tu ndio waweze kuiendesha kampuni hiyo.

No comments:

Post a Comment