Sunday 4 January 2015

SELENA GOMEZ AZUA KITAHANANI MSIKITINI




Selena Gomez visits Abu Dhabi's Sheikh Zayed Grand Mosque

Selena Gomez alizua kizaazaa wiki hii baada ya kuonyesha kiwiko chake alipotembelea msikiti – hatahivyo ameitoa picha hiyo baada ya kujikuta akikosolewa na wengi.

Alipigwa picha hiyo alipozuru msikiti mkubwa wa Sheikh Zayed, na alijistiri mwili mzima kwa ajili ya ziara hiyo.

Lakini ilipokuja wakati wa kupiga picha, Selena aliachia kiwiko na sehemu ya mguu hadharani.

Sheria za msikiti huo ziko wazi kuwa sketi zote lazima zifunike mpaka kiwiko, na unakataza ‘tabia zozote za kukaribiana ‘.

Mtu mmoja aliandika: "Kama nia yao ilikuwa kujifunza Uislamu wasingesimama kama wamesimama nje ya bustani.

Selena Gomez

"Nampenda Selena Gomez lakini kufanya jambo kama hili kunanifanya nisiwe mshabiki wake tena."

Mwengine aliongeza: "Si chuki. Lakini angetakiwa kuwa makini zaidi kuhusu misikiti. Ile sehemu ni takatifu na eneo la kuswali. Si sehemu ya kustarehe na kuchukua picha.

Lakini wapo wengine waliomtetea nyota huyo, mmoja akiandika: "Sio kwamba wamewavunjia heshima. Maelfu ya watu hutembelea msikiti huo wa Sheikh Zayed huko Abu Dhabi.

"Ni sehemu ya ibada, ndio najua, lakini Mungu hajawahi kukataza watu wa dini nyingine kuingia msikitini. Kwahiyo tafadhali heshimu kuwa walitaka kujua zaidi kuhusu Uislamu na uzuri wa dini hiyo."

Selena Gomez na muigizaji na mwimbaji kutoka Marekani ambaye pia aliwahi kuwa mpenzi wa muimbaji maarufu Justin Bieber.


Chanzo: www.mirror.co.uk                               
Imetafsiriwa na mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment