Friday 9 January 2015

VIONGOZI WA DINI YA KIISLAM 'WATOWEKA' UGANDA



A woman mourns the shooting of a Muslim cleric in Kampala, Uganda - December 2014

Viongozi wanne wa Kiislamu katika mji mkuu wa Uganda, Kampala wametoweka baada ya kuchukuliwa na watu wasioweza kutambuliwa, kiongozi wa jumuiya alisema.

Mkuu wa kundi la Kiiislamu la Tabliq aliiambia BBC “walitekwa” kutoka nyumbani kwao au sehemu za kazi.

Polisi bado hawajaanza kufanya uchunguzi kwani bado haijaripotiwa rasmi kuwa wametoweka, msemaji aliiambia BBC.

Haiko wazi kama kutoweka kwao kuna uhusiano na kupigwa risasi kwa viongozi wawili wa Kiislamu mwezi Desemba.

Mmoja alikuwa mkuu wa jumuiya ya Kishia ya Uganda, ambaye alipigwa risasi mashariki mwa Uganda na watu walio kwenye pikipiki Desemba 25, mwengine alikuwa kiongozi wa Tabliq aliyepigwa risasi kwenye gari lake Desemba 28 mjini Kampala.

Polisi wamenyooshea kidole mauaji hayo kwa waliobaki katika kundi la Allied Democratic Forces (ADF), kundi la waasi la Uganda lenye makao yake makuu nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Kundi hilo linaongozwa na Jamil Mukulu, ambaye kabla ya kuanza vuguvugu hilo, alikuwa kiongozi mwenye msimamo mkali ndani ya kundi la Tabliq katika miaka ya 90.

Mwandishi wa BBC alisema kumekuwa na mgongano wa uongozi ndani ya jumuiya ya Tabliq.

Viongozi wa Tabliq ambao hawajulikani walipo:

Yusuf Kakande, Siraj Kawooya , Twaha Ssekitto na Abdul Salam Sekayengo

Viongozi waliouawa mwezi Desemba:

Abdu Kadir Muwaya, kiongozi wa Kishia – aliipinga ADF
Sheikh Mustafa Bahiga, kiongozi wa Tabliq – aliyekuwa polisi na kuhusishwa katika mzozo wa uongozi ndani ya kundi hilo.


No comments:

Post a Comment