Tuesday 13 January 2015

TOVUTI MPYA YAUNDWA KUFICHUA SIRI ZA AFRIKA



 Young Ivorian learn how to use a computer on 22 April 2004 in Abidjan

Tovuti  inayofichua mambo yaliyojificha uliolilenga hasa bara la Afrika umeanzishwa, ukikusudia kuimarisha mapambano dhidi ya rushwa barani humo.

Imeahidi kuficha utambulisho kwa yeyote atakayetaka kutoa taarifa za siri kwa magazeti huru.

Tovuti hiyo - inayoitwa afriLeaks - imesema inataka kuwaunganisha wafichuaji maovu na kundi la waandishi wa habari wanaofichua  na kuandika habari za uchunguzi, na pia kutoa mafunzo maalum kwa waandishi hao.

Makundi ya vyombo vya habari Zimbabwe, Msumbiji, Angola na Botswana tayari washajiunga na mtandao huo.  

Afrika limekua kwa kasi kiuchumi katika miaka ya hivi karibuni lakini idara nyingi zinabaki kuwa dhaifu, na rushwa inakisiwa kuigharimu bara hilo mabilioni ya dola kila mwaka.

Afrileaks, iliyoundwa kutokana na vyombo vya habari 19 na makundi ya kutetea haki za binadamu, imedhamiria “kueleza ukweli “.

Miongoni mwa 19 mengi ni magazeti likiwemo la Afrika kusini Mail & Guardian, Daily Nation la Kenya na  Premium Times la Nigeria.

Nia hasa ni kuwafichua wanasiasa na wafanyabiashara barani humo wanaotumia vibaya madaraka yao.

Chanzo: theguardian.com

No comments:

Post a Comment