Tuesday 13 January 2015

'MAAMUZI' YA GRACE MUGABE YAZUIWA MAHAKAMANI



A Zimbabwean villager weeps in front of burning and demolished makeshift shelters at Manzou Farm in Mazowe - 8 January 2015

Mahakama kuu ya Zimbabwe imesimamisha hatua ya kuondoshwa kwa zaidi ya familia 200 kwenye shamba lililopo kaskazini mwa nchi hiyo hadi kutakapokua na nyumba mbadala kwa ajili yao.

Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu wamemshutumu mke wa rais wa nchi hiyo, Grace Mugabe, kutaka kubadilisha shamba hilo kuwa hifadhi ya wanyama.

Afisa mmoja amekana kuwa Bi Mugabe ana uhusiano wowote na eneo hilo.

Hata hivyo familia hizo zinasisitiza waliambiwa na polisi waondoke ili kumpisha Rais Robert Mugabe na mke wake.

No comments:

Post a Comment