Friday 9 January 2015

YAYA TOURE: MCHEZAJI BORA AFRIKA





Kiungo wa Manchester City Yaya Toure amekuwa mchezaji wa kwanza kutajwa kuwa mshindi wa tuzo ya CAF  wa mchezaji bora wa Afrika kwa miaka minne mfululizo.

Toure, mwenye umri wa miaka 31, alitajwa kuwania tuzo hiyo baada ya kuchangia kwa kiasi kikubwa kushinda Ligi Kuu ya England na Kombe la Ligi.

Pia aliisaidia Ivory Coast kufuzu kucheza kwa Kombe la Mataifa ya Afrika 2015.

Toure ameweza kuwashinda mshambuliaji wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang na mlinda mlango wa Nigeria Vincent Enyeama.

Kiungo Toure alitajwa miongoni mwa wachezaji wa kuwania tuzo ya Ballon D’Or  2014 ya Fifa mwezi Oktoba.

No comments:

Post a Comment