Friday 16 January 2015

MAFURIKO YAUA TAKRIBAN 170 MALAWI


Malawians displaced by floods

Serikali ya Malawi imesema takriban watu 170 wamefariki dunia kutokana na mafuriko – ongezeko kubwa sana.

Mvua kubwa katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita umevurumusha nyumba tele na kusababisha wakazi wengi kuhamia uwanda wa juu, wengine wakivuka mpaka hadi Msumbiji.

Makamu wa rais Saulos Chilima alisema zaidi ya watu 100,000 walihama makazi yao, hasa kusini.
Mapema wiki hii, serikali ilitangaza kuwa theluthi ya nchi hiyo ni eneo la majanga na kuomba msaada.

Mamlaka za Malawi zimekuwa zikitumia helikopta za kijeshi na boti kuwafikia baadhi ya watu waliokwama.

Lakini Bw Chilima alisema shughuli za uokoaji zinakwama kutokana na hali mbaya ya hewa katika siku chache zilizopita na ugumu wa kupata sehemu ya kutua kwa helikopta hizo.

No comments:

Post a Comment