Wednesday 7 January 2015

'KAMANDA' WA LRA AJISALIMISHA CAR



Dominic Ongwen (2008 file image)
Ongwen, picha ya mwaka 2008, inasemekana alichukuliwa kuwa jeshi la LRA tangu akiwa mtoto

Mtu mmoja anayedai kuwa kamanda mwandamizi katika kundi kubwa la waasi la Lord's Resistance Army (LRA) ametiwa kizuizini na jeshi la Marekani.

Mtu huyo, aliyejitambulisha kama Dominic Ongwen,alisalimu amri Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, wizara ya mambo ya nje ya Marekani ilisema.

Ongwen anasakwa na Mahakama ya Uhalifu wa Kivita akishutumiwa kuhusika na uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.

Anadhaniwa na baadhi ya watu kuwa naibu kamanda wa kiongozi wa LRA Joseph Kony.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani Jen Psaki alisema mtu huyo alidai kuwa ameasi kundi hilo la LRA.
Joseph Kony, kiongozi wa LRA wamekuwa vitani nchini Uganda na eneo zima kwa zaidi ya miongo miwili.

Chanzo: BBC
Imetafsiriwa na mwandishi wetu

No comments:

Post a Comment